Shekha Manjano ni mmiliki wa kampuni ya vipodozi vya manjano na juzi aliweka beauty tip ya namna ambavyo una weza kutumia manjano,mtindi,ndimu na asali kuondoa chunusi.. na hivi ndivyo alivyo andika katika kutoa somo hilo
“Weekend yangu naimalizia kujipamper na homemade face mask. Kama unasaumbuliwa na chunusi, au unauso wenye mafuta mengi kama wangu basi mara moja kwa wiki tengeneza ‘Face Mask’ yako mwenyewe nyumbani ili kupata ngozi soft.
Vifaa vinavyohitajika ni kama ifuatavyo;
Mimi hupendelea Zanzibar Turmeric Powder. Hii ni binzari ya Manjano hupatikana masokoni na supermarmets. –
Vijiko viwili (2 tbs) vya unga wa binzari ya Manjano (Turmeric powder)
– Kijiko kimoja (1 tbs) cha unga wa Riwa – wengine huita Liwa (Sandalwood powder)
– Vijiko vitatu (3 tbs) Mtindi (yoghurt)
– Nusu kijiko (1/2 tbs) maji ya ndimu (lemon juice)
– Kijiko kimoja (1 tbs) Asali ya bibi (honey)
Kwanza safisha uso wako kwa sabuni uwe msafi.
Changanya vyote kisha upake usoni (kasoro eneo lililozunguka jicho). Kaa nayo usoni mpaka ikauke au kwa muda wa dakika 10 – 15.
Kisha nawa uso wako kwa maji ya vuguvugu – usitumie sabuni.
Kama unazo chunusi nyingi, fanya hivi mara 3 kwa wiki na utaona mafanikio ya chunusi kuisha kabisa. Vilevile kama chunusi ulizonazo ni za muda mrefu, unaweza chukua glasi moja ya maziwa ‘fresh’; weka kijiko kimoja (tea spoon) cha unga wa binzari ya Manjano, vijiko viwili vya asali ya bibi, koroga na unywe – kunywa mara 3 kwa wiki (sio kila siku) – Itasaidia kuboost ‘immunity’ yako na pia kuisaidia system yako mwilini katika kutibu chunusi.
Kama huna chunusi kabisa fanya kujitengenezea face mask mara moja kwa wiki maana hii ni kinga hasa kama una uso wa mafuta (oily skin).
Related posts
3 Comments
Leave a Reply Cancel reply
You must be logged in to post a comment.
HOT TOPICS
Subscribe for newsletter
* You will receive the latest news and updates on your favorite celebrities!
Interviews
Fahamu Zaidi Kuhusu Vazi La Vijiko Kutoka Kwa Harmonize
Mwanamuziki Harmonize ametoa wimbo wake mpya uitwao Attitude, katika music video ya wimbo huu Harmonize ameonekana akiwa amevalia vazi la leather lenye vijiko, uma na visu ( silverware/ cutlery ) Vazi hili limeonekana ku-trend sana wengine wakiwa wanalisifia na wengine kuliponda, tumemtafuta stylist na mbunifu…
Maoni Ya Mbunifu Elisha Red Label Kuhusu Event Ya Miss Tanzania 2020
Tanzania imepata mlimbwende wake mpya ambae ataenda kuliwakilisha Taifa mwakani katika mashindano ya Dunia ya urembo. Tumeona sio mbaya kama tukifanya mahojiano na baadhi ya wabunifu, makeup artist na stylist ambao wametupa maoni yao kuhusu event hii. Hapa tunae mbunifu mkubwa wa mavazi ya kike…
Meet Eddie A Young Male Makeup Artist In A Female Dominated Industry
Anaitwa Eddie ( Makeup By Eddie ) ni mvulana ambae anafanya vizuri katika tasnia ya urembo, Eddie ni makeup artist tofauti na wengine Eddie yeye ni mvulana na kama ambavyo tunajua tasnia hii imetawaliwa sana na wanawake katika bara letu la Africa. Tumepata kujua mawili…
Husiyo Yajua Kuhusu Vaazi
Weekend hii tuliweza shuhudia maonyesho ya mavazi katika Tanzania Summer Festival iliyofanyika pale Double Tree Hotel. Tulivutiwa sana na kazi ya mbunifu chipukizi [pia stylist Vaazi na hivyo kuongea naye mwawili matatu juu ya kazi zake. AFRO: Umetambulika kama stylist anayechipukia na kufanya vizuri, waweza…
… [Trackback]
[…] Find More on that Topic: afroswagga.com/urembo/manjanoasalindimu-na-mtindi-facial-mask/ […]
… [Trackback]
[…] Read More here to that Topic: afroswagga.com/urembo/manjanoasalindimu-na-mtindi-facial-mask/ […]
… [Trackback]
[…] Read More here to that Topic: afroswagga.com/urembo/manjanoasalindimu-na-mtindi-facial-mask/ […]