Soko la urembo linazidi kukua Duniani, tunaona makampuni mapya ya vipodozi yakizinduliwa siku mpaka siku, watu maarufu pia wanaonekana kuvutiwa na soko hili.
Kama ilivyo kawaida kila jambao linapande mbili kuna wale watakao vutiwa nalo na wale ambao hawatotaka liendelee hata kidogo.
Week chache zilizopita wasanii wawili maarufu wa hiphop Madee Ally na Nikki wa Pili walitoa maoni yao kuhusu urembo wa makeup ambao wote wawili wakiwa na mitazamo hasi kuhusu urembo huo.
Ambapo alieanza ni Nikki wa pili ambae alisema yeye kwa upande wake anaona ma’bibi harusi wengi wakipaka makeup hawapendezi

Sisi hatujajua Nikki amewaona ma’bibi harusi gani au wa wapi, kwa sababu asilimia kubwa ya ma’bibi harusi huwa wanarembwa na wakarembeka hasa unless otherwise Nikki aliongea haya akiwa ameona wale mabibi harusi ambao hupakwa powder za baby Johson. Kama ukipata makeup artist ambae ni mzuri definitely utapakwa makeup na ukapendeza vyema kabisa.
Wakati Madee Ally yeye ugomvi wake ulikuwa na wanawake ambao wakiingia ndani ya ndoa wanaanza kujipodoa , akisema wanaume wengi wanasaliti (cheat) kwa sababu tu wakati anakuona hukuwa na kucha bandia, nywele bandia lakini baada ya kuwa nae umeanza kuweka hivyo vitu.

Neno letu ni moja tu kwa bwana Madee, mwanaume au mwanamke akitaka kukusaliti atakusaliti uwe natural kama uoto wa asili au ujibandike as long as anataka kucheat basi ata-cheat. Ni kama umwambie mwanaume wanawake wanacheat sababu wakati unakuwa nae ulikuwa na nywele na six pack lakini baada ya kuwa nae umekuwa na upara na kitambi.
Related posts
HOT TOPICS
We need to have some sort of bima ila for enjoyment. Yaani wanakata ka % ka mshahara kako unakua na card ukienda se… https://t.co/W9oDoaN2YY
FollowSubscribe for newsletter
* You will receive the latest news and updates on your favorite celebrities!
Interviews
Fahamu Zaidi Kuhusu Vazi La Vijiko Kutoka Kwa Harmonize
Mwanamuziki Harmonize ametoa wimbo wake mpya uitwao Attitude, katika music video ya wimbo huu Harmonize ameonekana akiwa amevalia vazi la leather lenye vijiko, uma na visu ( silverware/ cutlery ) Vazi hili limeonekana ku-trend sana wengine wakiwa wanalisifia na wengine kuliponda, tumemtafuta stylist na mbunifu…
Maoni Ya Mbunifu Elisha Red Label Kuhusu Event Ya Miss Tanzania 2020
Tanzania imepata mlimbwende wake mpya ambae ataenda kuliwakilisha Taifa mwakani katika mashindano ya Dunia ya urembo. Tumeona sio mbaya kama tukifanya mahojiano na baadhi ya wabunifu, makeup artist na stylist ambao wametupa maoni yao kuhusu event hii. Hapa tunae mbunifu mkubwa wa mavazi ya kike…
Meet Eddie A Young Male Makeup Artist In A Female Dominated Industry
Anaitwa Eddie ( Makeup By Eddie ) ni mvulana ambae anafanya vizuri katika tasnia ya urembo, Eddie ni makeup artist tofauti na wengine Eddie yeye ni mvulana na kama ambavyo tunajua tasnia hii imetawaliwa sana na wanawake katika bara letu la Africa. Tumepata kujua mawili…
Husiyo Yajua Kuhusu Vaazi
Weekend hii tuliweza shuhudia maonyesho ya mavazi katika Tanzania Summer Festival iliyofanyika pale Double Tree Hotel. Tulivutiwa sana na kazi ya mbunifu chipukizi [pia stylist Vaazi na hivyo kuongea naye mwawili matatu juu ya kazi zake. AFRO: Umetambulika kama stylist anayechipukia na kufanya vizuri, waweza…