Weekends ni muda mzuri wa kujijali mwenyewe, kwenda salon kuosha na kusafisha nywele, kujali kucha zako, kupumzika lakini pia ni muda mzuri wa kujali ngozi yako. Week nzima una amka asubuhi na kwenda kazini unatembea juani na kukosa muda wa kujijali ila inapofikia weekend basi inabidi uvijali vile vyote ambavyo hukuweza kufanya.
Leo tumewaletea namna unavyo weza kutumia mmea wa Aloe Vera (m-shubiri) kutibu ngozi yako kwa kuondoa alama nyeusi zilizo takana na chunusi au kuungua na jua. Aloe Vera Ina anthra-quinone ambayo husaidia kuondoa dead skin cells naturally, hii hupelekea kusafisha na kung’aza ngozi na kutibu tatizo lolote la ngozi zikiwepo chunusi na madoa yaliyo tokana na chunusi
Aloe – vera ina faida nyingi katika ngozi na hutibu magonjwa mengi ya ngozi lakini leo tunawaletea njia 3 za namna unaweza kutumia Aloe – Vera kuondoa weusi katika ngozi.
Vitamin E na Aloe Vera Gel ( Ute wa mshubiri/aloe vera)
Mahitaji:
- Ute wa Aloe Vera – kijiko kimoja
- Vitamin E – Nusu Kijiko
Namna Ya Kufanya
- Changanya mahitaji yako kwa pamoja, unaweza kutumia Vitamin E oil au kutumia vidonge kivunje katikati na changanya na ute wa aloe vera mpaka kiyeyuke
- Safisha uso wako kwa kutumia chochote ambacho unatumiaga kusafishia kila siku na taratibu chukua mchanganyiko wako upake kwenye madoa na uanze ku massage sehemu hio
- uache mchanganyiko wako ukauke huchukua takribadi dakika 30-35
- Osha/Safisha sehemu uliyo paka mchanganyiko wako na uache ngozi ipumue.
- Fanya hivi mara mbili kwa week kupata matokeo bora mapema.
Asali Na Aloe Vera Gel ( Ute Wa Mshubiri/Aloe vera)
Mahitaji
Namna Ya Kuandaa
- Changanya mahitaji yako kwa pamoja
- Safisha uso wako kwa kutumia chochote ambacho unatumiaga kusafishia kila siku na taratibu chukua mchanganyiko wako upake kwenye madoa na uanze ku massage sehemu hio
- iache ikauke katika ngozi yako kwa muda wa dakika 20-25
- safisha uso wako kwa maji ya uvugu vugu na iache ngozi ipumue kwa muda kabla ya kupaka vipodozi vyako.
- fanya hivi mara mbili kwa week kupata matokeo bora.
Limao/Ndimu na Aloe Vera Gel
Mahitaji:
- Aloe Vera Gel – vijiko vitatu
- Ndimu – Kijiko Kimoja
- Asali – Vijiko Viwili
Namna Ya Kuandaa
- Changanya mahitaji yako kwa pamoja
- Safisha uso wako kwa kutumia chochote ambacho unatumiaga kusafishia kila siku na taratibu chukua mchanganyiko wako upake kwenye madoa na uanze ku massage sehemu hio
- acha mchanganyiko wako ukae kwa muda mrefu, unaweza kupakaa usiku ukalala nao ukisha kauka. Hii inasaidia sana endapo tu utakaa nayo kwa muda mrefu usoni
- Osha na ondoa mchanganyiko wako kwa maji ya baridi.
- Tumia njia hii kila siku kwa matokeo bora.
Related posts
4 Comments
Comments are closed.
HOT TOPICS
Subscribe for newsletter
* You will receive the latest news and updates on your favorite celebrities!
Interviews
Fahamu Zaidi Kuhusu Vazi La Vijiko Kutoka Kwa Harmonize
Mwanamuziki Harmonize ametoa wimbo wake mpya uitwao Attitude, katika music video ya wimbo huu Harmonize ameonekana akiwa amevalia vazi la leather lenye vijiko, uma na visu ( silverware/ cutlery ) Vazi hili limeonekana ku-trend sana wengine wakiwa wanalisifia na wengine kuliponda, tumemtafuta stylist na mbunifu…
Maoni Ya Mbunifu Elisha Red Label Kuhusu Event Ya Miss Tanzania 2020
Tanzania imepata mlimbwende wake mpya ambae ataenda kuliwakilisha Taifa mwakani katika mashindano ya Dunia ya urembo. Tumeona sio mbaya kama tukifanya mahojiano na baadhi ya wabunifu, makeup artist na stylist ambao wametupa maoni yao kuhusu event hii. Hapa tunae mbunifu mkubwa wa mavazi ya kike…
Meet Eddie A Young Male Makeup Artist In A Female Dominated Industry
Anaitwa Eddie ( Makeup By Eddie ) ni mvulana ambae anafanya vizuri katika tasnia ya urembo, Eddie ni makeup artist tofauti na wengine Eddie yeye ni mvulana na kama ambavyo tunajua tasnia hii imetawaliwa sana na wanawake katika bara letu la Africa. Tumepata kujua mawili…
Husiyo Yajua Kuhusu Vaazi
Weekend hii tuliweza shuhudia maonyesho ya mavazi katika Tanzania Summer Festival iliyofanyika pale Double Tree Hotel. Tulivutiwa sana na kazi ya mbunifu chipukizi [pia stylist Vaazi na hivyo kuongea naye mwawili matatu juu ya kazi zake. AFRO: Umetambulika kama stylist anayechipukia na kufanya vizuri, waweza…
… [Trackback]
[…] Find More on on that Topic: afroswagga.com/urembo/namna-3-za-kutumia-aloe-vera-kuondoa-madoa-katika-ngozi/ […]
… [Trackback]
[…] Information to that Topic: afroswagga.com/urembo/namna-3-za-kutumia-aloe-vera-kuondoa-madoa-katika-ngozi/ […]
… [Trackback]
[…] Read More to that Topic: afroswagga.com/urembo/namna-3-za-kutumia-aloe-vera-kuondoa-madoa-katika-ngozi/ […]
… [Trackback]
[…] Find More here to that Topic: afroswagga.com/urembo/namna-3-za-kutumia-aloe-vera-kuondoa-madoa-katika-ngozi/ […]