Kwanza kabisa naanza na kesi ya madoadoa mwilini. Iwe ya usoni yaliyotokana na chunusi au Sehemu zingine za mwili kutokana na upele, vidonda na kadhalika.
Katika mazingira kama hayo ushauri ufuatao utakufaa:
- Kadiri muda unavyoenda ngozi yako Itakuwa inajitengeneza vizuri yenyewe na hivyo madoadoa hayo yatakuwa yanafifia Pole Pole na hata hatimaye kupotea kabisa kutegemea na umri wako, lishe yako, ulipata ukiwa na umri gani na ni madoadoa au makovu ya ukubwa gani.
Ukiwa na umri mdogo mwili hukua na kufanya ukarabati haraka haraka hivyo madoadoa huwai kupungua na kuisha; ukiwa unakula vizuri nyama, mayai, maziwa, maini, samaki, kuku, maharage na vyakula vingine vya protini unapata protini ya kutosha na madoadoa yanawahi kuisha; madoadoa madogomadogo yanawahi kufifia na kuisha; kwa hiyo unaweza kula vizuri na kuwa mvumilivu tu na madoadoa yako yakapungua na kuisha…..
- Unaweza kuharakisha madoadoa kuisha kwa kutumia vipodozi ambazo husaidia ngozi kujitengeneza upya na kuondoa ngozi ya zamani yenye madoadoa. Bio oil ni miongoni mwa dawa na vipodozi ambavyo husaidia kupunguza na kuondoa madoadoa na makovu. Unachotakiwa kufanya ni kuwa makini sana na utumiaji na kununua kutoka kwa wauzaji wanaoaminika
Faida Na Matumizi Ya Mafuta Ya Bio-Oil
- Kupaka make-up na makorokoro mengine ili kuficha madoadoa ni kupoteza pesa nyingi maana haiondoa madoadoa na bado gharama yake ni kubwa kiasi cha kutosha kuondoa kabisa madoadoa yako
Kwa kusema ukweli kila tatizo la ngozi, lina vipodozi vya kulimaliza; isipokuwa tu watu wanakosa matokeo mazuri kwa sababu ya kufuata ushauri mbaya na kutotumia vipodozi maalum kwa ajili ya tatizo husika na ngozi husika
Kwa hiyo kama unasumbuliwa na madoadoa Leo nakupa nguvu na uhakika kwamba unaweza kumaliza madoadoa yako yote, kupendeza na kung’aa kama zamani
Usitumie vipodozi vikali, hakuna haja ya kuharibu ngozi yako nzuri kwa fedha yako mwenyewe wala kujificha kwa Hijabu, Suruali na Make Up
Pata ushauri mzuri, kuwa chini ya muangalizi mwenye uelewa mzuri wa vipodozi na tumia bidhaa nzuri. Kingine Uwe mvumulivu!
Baada ya hapo utapata matokeo yoyote mazuri unayoyataka.
Related posts
HOT TOPICS
We need to have some sort of bima ila for enjoyment. Yaani wanakata ka % ka mshahara kako unakua na card ukienda se… https://t.co/W9oDoaN2YY
FollowSubscribe for newsletter
* You will receive the latest news and updates on your favorite celebrities!
Interviews
Fahamu Zaidi Kuhusu Vazi La Vijiko Kutoka Kwa Harmonize
Mwanamuziki Harmonize ametoa wimbo wake mpya uitwao Attitude, katika music video ya wimbo huu Harmonize ameonekana akiwa amevalia vazi la leather lenye vijiko, uma na visu ( silverware/ cutlery ) Vazi hili limeonekana ku-trend sana wengine wakiwa wanalisifia na wengine kuliponda, tumemtafuta stylist na mbunifu…
Maoni Ya Mbunifu Elisha Red Label Kuhusu Event Ya Miss Tanzania 2020
Tanzania imepata mlimbwende wake mpya ambae ataenda kuliwakilisha Taifa mwakani katika mashindano ya Dunia ya urembo. Tumeona sio mbaya kama tukifanya mahojiano na baadhi ya wabunifu, makeup artist na stylist ambao wametupa maoni yao kuhusu event hii. Hapa tunae mbunifu mkubwa wa mavazi ya kike…
Meet Eddie A Young Male Makeup Artist In A Female Dominated Industry
Anaitwa Eddie ( Makeup By Eddie ) ni mvulana ambae anafanya vizuri katika tasnia ya urembo, Eddie ni makeup artist tofauti na wengine Eddie yeye ni mvulana na kama ambavyo tunajua tasnia hii imetawaliwa sana na wanawake katika bara letu la Africa. Tumepata kujua mawili…
Husiyo Yajua Kuhusu Vaazi
Weekend hii tuliweza shuhudia maonyesho ya mavazi katika Tanzania Summer Festival iliyofanyika pale Double Tree Hotel. Tulivutiwa sana na kazi ya mbunifu chipukizi [pia stylist Vaazi na hivyo kuongea naye mwawili matatu juu ya kazi zake. AFRO: Umetambulika kama stylist anayechipukia na kufanya vizuri, waweza…