Madoa meusi (black spots) usoni ni jambo ambalo linawasumbua wanawake wengi sana na hupelekea mtu kutokujiamini na mara nyingine kujidharau, kujichukia na kukosa ujasiri wa kuwa bila ya make up “off make up”. Hili tatizo husabaishwa na vitu tofauti,hivyo kujua chanzo cha tatizo ni muhimu sana.
Sababu zinazosababisha madoa meusi usoni ni kama ifuatavyo;
1.Hyperpigmentation
Hili tatizo linatokea pale ngozi inapoharibiwa katika eneo fulani,hivyo husababisha ngozi kutengeneza ‘melanin’ nyingi na kusababisha eneo hilo kuonekana nyeusi kuliko nyingine.
2.Homoni kutokuwa katika kiwango sahihi katika mwili(Hormonal imbalances)
Pia hili husababisha madoa meusi usoni, na hili linaweza tokea wakati wa ujauzito,kwa watu wanaotumia vidonge vya uzazi wa mpango(control pills) na pia mwanamke anapoingia katika kipindi cha ukomo wa kuzaa(menopause).
3.Kukaa juani kwa muda mrefu(excessive sun exposure).
Pia hii hutokea kwasababu mwili unaanza kutengeneza ‘melanin’ kwa wingi ili kuzuia kuharibiwa kwa ngozi na mionzi ya jua. Na hapo Ndio utaona madoa meusi usoni
4.Chunusi
Pia hutokea kwa watu ambao wana tatizo la chunusi. Wengi wenye chunusi huwa na tabia ya kutumbua chunusi na Kwa kufanya hivyo chunusi hupona kwa kubakiza kovu jeusi usoni. Mara nyingi haya madoa meusi yanapotea baada ya muda fulani kupita,lakini muda mwingine inaweza ikawa ni ngumu kupotea yenyewe kutokana na aina hizo za chunusi. Na Hapo Ndio Mwanamke huanza kujichukia na kujiona Hafai.
Kama Umekuwa na tatizo hili kwa muda mrefu, usijali Leo hapa hapa utajua nini cha kufanya ukiwa nyumbani kwako.
Jinsi ya kuondoa madoa meusi ukiwa nyumbani
- Tumia juice ya aloe vera
paka sehemu yenye madoa meusi mara mbili kwa siku. Fanya hivi kwa wiki kadhaa na utashuhudia mabadiriko makubwa.

- Asali na sukari
Changanya asali na sukari hii ya kawaida na ujifanyie ‘massage’ mara mbili kwa wiki. Hii husaidia kuondoa chembechembe za ngozi zilizokufa na kufanya ngozi mpya na hivyo kuondoa madoa meusi.
Njia Asili Ya Kuondoa Madoa Yaliyo Tokana Na Chunusi
- Tumia matunda ambayo yana uwingi wa vitamin C na E
Matunda kama machungwa yana vtamin C ambavyo ni Antioxydant na pia hupunguza melanin isitengenezwe kwa wingi na hivyo kufanya ngozi isiwe na madoa meusi. Pia matunda ambayo yana vitamin E kwa wingi ni muhimu kuyatumia ,mfano Carrots.

- Tumia sunscreen cream
.Hizi cream huzuia mionzi ya jua ambayo ni chanzo mojawapo cha madoa meusi usoni, kwa hiyo hakikisha unatumia sunscreen cream kabla ya kutoka kwa ajili ya matembezi ya hapa na pale.
Hizo ni “home remedies” huleta matokeo mazuri sana, ila bahati mbaya hayaji kwa muda mfupi. Unatakiwa kuwa Mwaminifu na mvumilivu!
Umuhimu Wa Kupaka Sunscreen Katika Ngozi
Pia ukiona madoa yako hayatoki unaweza ukamwona mtaalam wa ngozi kwa ajili ya ushauri na matibabu zaidi.
Jee ni nini utafanya Kati ya hayo tuliyoeleza Hapo juu!? Tuambie kwenye Comment hapo chini.
Related posts
5 Comments
Comments are closed.
HOT TOPICS
Subscribe for newsletter
* You will receive the latest news and updates on your favorite celebrities!
Interviews
Fahamu Zaidi Kuhusu Vazi La Vijiko Kutoka Kwa Harmonize
Mwanamuziki Harmonize ametoa wimbo wake mpya uitwao Attitude, katika music video ya wimbo huu Harmonize ameonekana akiwa amevalia vazi la leather lenye vijiko, uma na visu ( silverware/ cutlery ) Vazi hili limeonekana ku-trend sana wengine wakiwa wanalisifia na wengine kuliponda, tumemtafuta stylist na mbunifu…
Maoni Ya Mbunifu Elisha Red Label Kuhusu Event Ya Miss Tanzania 2020
Tanzania imepata mlimbwende wake mpya ambae ataenda kuliwakilisha Taifa mwakani katika mashindano ya Dunia ya urembo. Tumeona sio mbaya kama tukifanya mahojiano na baadhi ya wabunifu, makeup artist na stylist ambao wametupa maoni yao kuhusu event hii. Hapa tunae mbunifu mkubwa wa mavazi ya kike…
Meet Eddie A Young Male Makeup Artist In A Female Dominated Industry
Anaitwa Eddie ( Makeup By Eddie ) ni mvulana ambae anafanya vizuri katika tasnia ya urembo, Eddie ni makeup artist tofauti na wengine Eddie yeye ni mvulana na kama ambavyo tunajua tasnia hii imetawaliwa sana na wanawake katika bara letu la Africa. Tumepata kujua mawili…
Husiyo Yajua Kuhusu Vaazi
Weekend hii tuliweza shuhudia maonyesho ya mavazi katika Tanzania Summer Festival iliyofanyika pale Double Tree Hotel. Tulivutiwa sana na kazi ya mbunifu chipukizi [pia stylist Vaazi na hivyo kuongea naye mwawili matatu juu ya kazi zake. AFRO: Umetambulika kama stylist anayechipukia na kufanya vizuri, waweza…
… [Trackback]
[…] Info on that Topic: afroswagga.com/urembo/namna-ya-kuondoa-madoa-meusi-usoni/ […]
… [Trackback]
[…] Read More on that Topic: afroswagga.com/urembo/namna-ya-kuondoa-madoa-meusi-usoni/ […]
… [Trackback]
[…] Find More on on that Topic: afroswagga.com/urembo/namna-ya-kuondoa-madoa-meusi-usoni/ […]
… [Trackback]
[…] Find More here on that Topic: afroswagga.com/urembo/namna-ya-kuondoa-madoa-meusi-usoni/ […]
… [Trackback]
[…] Find More to that Topic: afroswagga.com/urembo/namna-ya-kuondoa-madoa-meusi-usoni/ […]