Watu wengi wana uchafu kwenye ngozi hata wakioga bila kujua sababu ni nini, wengine wanakuwa na weusi flani hata kama ni mweupe. Utasikia mtu anasema flani haogi vizuri, siyo kweli ni ngozi inakuwa imechoka.
Scrub nzuri ya kuondoa weusi huo ni sukari na mafuta ya mzaituni ambayo inapakwa kisha unafanyia masaji mwili mzima kuondoa uchafu wa ngozi.

Jinsi ya kuandaa
- Chukua kahawa vijiko viwili vikubwa,
- kijiko 1 kikubwa cha sukari
- mafuta ya mzaituni vijiko vinne.
Changanya vyote kwa pamoja upate mchanganyiko. Baada ya hapo, chukua mchanganyiko huo paka mwilini mwako, ufanyie mwili masaji kama unayesugua sehemu hasa sehemu nyeusi, zoezi hilo lifanye wakati unaoga.
Nikisema sehemu nyeusi namaanisha kwenye maungio, makwapani na shingoni, hizi ni sehemu ambazo weusi wake huwa unazidi hivyo kwa kutumia mchanganyiko huu unaweza kurudisha rangi asili ya ngozi yako.
Kwa wanaotaka kung’arisha miguu scrub hii pia ni nzuri, inafaa kwa asilimia kubwa. Scrub hii inafaa kwa sehemu yote ya mwili isipokuwa usoni tu.
Vile vile Kahawa ina matumizi mengine Kama kuondoa michirizi na chunusi Kama ifuatavyo :

Scrub ya Kahawa kwa michirizi.
Chukua Kahawa na mafuta ya Nazi , changanya vizuri kisha itumie kama scrub nyingine katika sehemu ambapo una michirizi.
Scrub pole pole kwa kuzunguka “circular motion” kwa Muda wa dakika 10-15. Kisha nawa kwa maji ya uvuguvugu. Kausha Kisha paka moisturizer.
Scrub ya kawaha kuondoa Chunusi.

Vitu unavyohitaji ni Kahawa Mafuta ya Nazi Na Mdalasini.
Changanya vizuri kiasi sawa kwa Kila kitu.
Paka usoni na uwe kama unasugua polepole kwa Muda wa dakika 5-10.
Nawa uso kwa maji ya uvuguvugu Kisha paka moisturizer.
Fanya mara 2 kwa wiki kwa miezi 3. Utaona matokeo mazuri.
Wanatumia wenye ngozi Aina Zote na umri wowote!
Jee umewahi kutumia Kahawa Katika urembo, unatumiaje?
Shea na uwapendao
©binturembo
Unaweza kupata mafuta ya nazi bora kutoka kwetu @afroswaggaoils au tupigie kupitia 0765 768 667
Related posts
4 Comments
Comments are closed.
HOT TOPICS
Subscribe for newsletter
* You will receive the latest news and updates on your favorite celebrities!
Interviews
Fahamu Zaidi Kuhusu Vazi La Vijiko Kutoka Kwa Harmonize
Mwanamuziki Harmonize ametoa wimbo wake mpya uitwao Attitude, katika music video ya wimbo huu Harmonize ameonekana akiwa amevalia vazi la leather lenye vijiko, uma na visu ( silverware/ cutlery ) Vazi hili limeonekana ku-trend sana wengine wakiwa wanalisifia na wengine kuliponda, tumemtafuta stylist na mbunifu…
Maoni Ya Mbunifu Elisha Red Label Kuhusu Event Ya Miss Tanzania 2020
Tanzania imepata mlimbwende wake mpya ambae ataenda kuliwakilisha Taifa mwakani katika mashindano ya Dunia ya urembo. Tumeona sio mbaya kama tukifanya mahojiano na baadhi ya wabunifu, makeup artist na stylist ambao wametupa maoni yao kuhusu event hii. Hapa tunae mbunifu mkubwa wa mavazi ya kike…
Meet Eddie A Young Male Makeup Artist In A Female Dominated Industry
Anaitwa Eddie ( Makeup By Eddie ) ni mvulana ambae anafanya vizuri katika tasnia ya urembo, Eddie ni makeup artist tofauti na wengine Eddie yeye ni mvulana na kama ambavyo tunajua tasnia hii imetawaliwa sana na wanawake katika bara letu la Africa. Tumepata kujua mawili…
Husiyo Yajua Kuhusu Vaazi
Weekend hii tuliweza shuhudia maonyesho ya mavazi katika Tanzania Summer Festival iliyofanyika pale Double Tree Hotel. Tulivutiwa sana na kazi ya mbunifu chipukizi [pia stylist Vaazi na hivyo kuongea naye mwawili matatu juu ya kazi zake. AFRO: Umetambulika kama stylist anayechipukia na kufanya vizuri, waweza…
… [Trackback]
[…] Info to that Topic: afroswagga.com/urembo/namna-ya-kuondoa-weusi-mwilini-kwa-kutumia-scrub-ya-kahawa/ […]
… [Trackback]
[…] Read More here on that Topic: afroswagga.com/urembo/namna-ya-kuondoa-weusi-mwilini-kwa-kutumia-scrub-ya-kahawa/ […]
… [Trackback]
[…] Information on that Topic: afroswagga.com/urembo/namna-ya-kuondoa-weusi-mwilini-kwa-kutumia-scrub-ya-kahawa/ […]
… [Trackback]
[…] Read More Info here to that Topic: afroswagga.com/urembo/namna-ya-kuondoa-weusi-mwilini-kwa-kutumia-scrub-ya-kahawa/ […]