Weusi chini ya macho unasababishwa na mambo mengi ikiwamo kukosa usingizi wa kutosha. Binadamu anatakiwa kulala masaa yasiyopungua 6 hadi 8, kuhakikisha ubora wa afya na Ngozi yake.
KULALA na kupumzika ni muhimu kwa kuwa na afya nzuri na muonekano mzuri. Hata hivyo, aghalabu huwa sio rahisi kuupata usingizi wa kutosha kila usiku na wakati mwingine utaona weusi usoni chini ya macho unapokosa usingizi. Hali hii pia husababisha ‘puffy eyes’ yaani uvimbe wa aina fulani katika sehemu karibu na macho.
- Viazi
Viazi vina asili ya enzymes zinaong’arisha ngozi, ambao husaidia kufifiza weusi chini ya macho.Weka kiazi kibichi katika hiyo sehemu ya machoni unaweza kukikata vipande vidogo vyembamba au kwa kusaga kupakaa rojo.Weka kwa 30 dakika kisha toa,osha uso kwa maji ya kawaida.
- Majani ya Nanaa “Mint”
Yaponde majani ya mint kidogo na pakaa chini macho hapo kwa dakika tano. Safisha uso kwa maji ya kawaida. Unaweza ukatumia majani ya mint ukachanganya na asali au olive oil kabla hujapakaa kwenye macho. Baada ya kuosha, paka ‘moisturizer’.

- Tea bags
Caffeine ilioko ndani ya majani ya chai ina uwezo wa kukazisha ngozi chini ya macho na pia huondoa kuungua na mbadiliko wa rangi. Baada ya kutumia tea bag yako weka kwenye friji ipate baridi. Kisha Chukua tea bags zako mbili kutoka kwa friji weka kwenye macho yako yakiwa yamefungwa kwa kuilaza kwa dakika 15.
- Rose water
Rose water ina vitamini kama A na C, Unapaswa kuyapaka hayo maji chini ya macho kwa dakika 10 kwa kutumia pamba.
- Matango
Kuweka vipande vya matango ya baridi kwenye kila jicho husaidia kuondoa uchovu, na husaidia kulainisha ngozi ya machoni. Matango pia hufanya kazi ya kukaza na kung’arisha uso, husaidia kuondoa mabadiliko ya rangi katika ngozi.
Ni vizuri zaidi kutumia Njia moja kwa muda ili uweze kujua ni ipi hasa inakufaa! Rudia hadi uone matokeo unayotaka!
Jee wewe Utachagua ipi, Kati ya hizo Hapo juu!? Tuambie zaidi kwenye comment hapo chini.
Imeandikwa na @binturembo
Related posts
4 Comments
Comments are closed.
HOT TOPICS
Subscribe for newsletter
* You will receive the latest news and updates on your favorite celebrities!
Interviews
Fahamu Zaidi Kuhusu Vazi La Vijiko Kutoka Kwa Harmonize
Mwanamuziki Harmonize ametoa wimbo wake mpya uitwao Attitude, katika music video ya wimbo huu Harmonize ameonekana akiwa amevalia vazi la leather lenye vijiko, uma na visu ( silverware/ cutlery ) Vazi hili limeonekana ku-trend sana wengine wakiwa wanalisifia na wengine kuliponda, tumemtafuta stylist na mbunifu…
Maoni Ya Mbunifu Elisha Red Label Kuhusu Event Ya Miss Tanzania 2020
Tanzania imepata mlimbwende wake mpya ambae ataenda kuliwakilisha Taifa mwakani katika mashindano ya Dunia ya urembo. Tumeona sio mbaya kama tukifanya mahojiano na baadhi ya wabunifu, makeup artist na stylist ambao wametupa maoni yao kuhusu event hii. Hapa tunae mbunifu mkubwa wa mavazi ya kike…
Meet Eddie A Young Male Makeup Artist In A Female Dominated Industry
Anaitwa Eddie ( Makeup By Eddie ) ni mvulana ambae anafanya vizuri katika tasnia ya urembo, Eddie ni makeup artist tofauti na wengine Eddie yeye ni mvulana na kama ambavyo tunajua tasnia hii imetawaliwa sana na wanawake katika bara letu la Africa. Tumepata kujua mawili…
Husiyo Yajua Kuhusu Vaazi
Weekend hii tuliweza shuhudia maonyesho ya mavazi katika Tanzania Summer Festival iliyofanyika pale Double Tree Hotel. Tulivutiwa sana na kazi ya mbunifu chipukizi [pia stylist Vaazi na hivyo kuongea naye mwawili matatu juu ya kazi zake. AFRO: Umetambulika kama stylist anayechipukia na kufanya vizuri, waweza…
… [Trackback]
[…] Find More on on that Topic: afroswagga.com/urembo/namna-ya-kuondoa-weusi-wa-macho-miwani-puffy-eyes/ […]
… [Trackback]
[…] Read More Info here to that Topic: afroswagga.com/urembo/namna-ya-kuondoa-weusi-wa-macho-miwani-puffy-eyes/ […]
… [Trackback]
[…] Information to that Topic: afroswagga.com/urembo/namna-ya-kuondoa-weusi-wa-macho-miwani-puffy-eyes/ […]
… [Trackback]
[…] Here you will find 63630 more Info on that Topic: afroswagga.com/urembo/namna-ya-kuondoa-weusi-wa-macho-miwani-puffy-eyes/ […]