Unaweza ukawa una penda kupika/kula bagia za dengu au chakula chochote kinacho pikwa kutokana na unga wa dengu bila kujua unaweza kutumia dengu hio hio katika kufanya ngozi yako ing’ae. Kama ambavyo binadamu tunategemeana na mimea na wanyama katika kupata mahitaji yetu basi ndivyo ilivyo katika mahitaji ya jikoni na urembo na afya, kuna vyakula ambavyo unaweza ukala lakini pia unaweza kutumia katika urembo.

Leo tunakupa tips chache za namna unavyo weza kutumia unga wa dengu kung’arisha ngozi yako.
Mahitaji
- Unga wa dengu vijiko viwili vya chai
Namna ya kuandaa
Weka unga wa dengu katika kibakuli au chombo kisafi, kisha vunja yai pembeni na utoe kiini ambacho utakichanganya na unga.
Koroga mpaka uhakikishe mchanganyiko huo umechanganyika na kulainika kabisa.
Baada ya hapo safisha uso wako kwa maji ya uvuguvugu kisha jikaushe kwa taulo au kitambaa kisafi.
Baada ya kuhakikisha uso wako uko safi paka mchanganyiko huo kwa kuusambaza uso mzima, ikiwezekana pia katika maeneo ya shingoni na pembezoni mwa masikio ili kuzifanya pia sehemu hizo kuwa zenye mvuto wa aina yake.
Kaa na mchanganyiko huo kwa dk-15 kisha futa/osha uso wako kwa maji ya uvuguvugu.
Namna Nyingine #2
Mahitaji
- Vijiko Vinne Vya Unga wa dengu
- Limao kijiko kimoja
- maziwa kijiko kimoja
Namna ya kuandaa
Changanya unga, maziwa na limao kisha paka usoni mwako au sehemu yoyote ambayo ungependa kung’arisha, massage hio sehemu kwa dakika kadhaa kisha acha mchaganyiko huo katika uso wako mpaka ukauke.
Ikisha kauka osha kwa maji ya vuguvugu.
Ukitumia na ukipata matokeo usisite kutujulisha.
Related posts
4 Comments
Leave a Reply Cancel reply
You must be logged in to post a comment.
HOT TOPICS
Subscribe for newsletter
* You will receive the latest news and updates on your favorite celebrities!
Interviews
Fahamu Zaidi Kuhusu Vazi La Vijiko Kutoka Kwa Harmonize
Mwanamuziki Harmonize ametoa wimbo wake mpya uitwao Attitude, katika music video ya wimbo huu Harmonize ameonekana akiwa amevalia vazi la leather lenye vijiko, uma na visu ( silverware/ cutlery ) Vazi hili limeonekana ku-trend sana wengine wakiwa wanalisifia na wengine kuliponda, tumemtafuta stylist na mbunifu…
Maoni Ya Mbunifu Elisha Red Label Kuhusu Event Ya Miss Tanzania 2020
Tanzania imepata mlimbwende wake mpya ambae ataenda kuliwakilisha Taifa mwakani katika mashindano ya Dunia ya urembo. Tumeona sio mbaya kama tukifanya mahojiano na baadhi ya wabunifu, makeup artist na stylist ambao wametupa maoni yao kuhusu event hii. Hapa tunae mbunifu mkubwa wa mavazi ya kike…
Meet Eddie A Young Male Makeup Artist In A Female Dominated Industry
Anaitwa Eddie ( Makeup By Eddie ) ni mvulana ambae anafanya vizuri katika tasnia ya urembo, Eddie ni makeup artist tofauti na wengine Eddie yeye ni mvulana na kama ambavyo tunajua tasnia hii imetawaliwa sana na wanawake katika bara letu la Africa. Tumepata kujua mawili…
Husiyo Yajua Kuhusu Vaazi
Weekend hii tuliweza shuhudia maonyesho ya mavazi katika Tanzania Summer Festival iliyofanyika pale Double Tree Hotel. Tulivutiwa sana na kazi ya mbunifu chipukizi [pia stylist Vaazi na hivyo kuongea naye mwawili matatu juu ya kazi zake. AFRO: Umetambulika kama stylist anayechipukia na kufanya vizuri, waweza…
… [Trackback]
[…] Read More Information here on that Topic: afroswagga.com/urembo/ngarisha-ngozi-kwa-kutumia-unga-wa-dengu/ […]
… [Trackback]
[…] Information to that Topic: afroswagga.com/urembo/ngarisha-ngozi-kwa-kutumia-unga-wa-dengu/ […]
… [Trackback]
[…] Read More to that Topic: afroswagga.com/urembo/ngarisha-ngozi-kwa-kutumia-unga-wa-dengu/ […]
… [Trackback]
[…] Read More Info here to that Topic: afroswagga.com/urembo/ngarisha-ngozi-kwa-kutumia-unga-wa-dengu/ […]