Katika shughuli za kila siku swala la miili yetu kupatwa na mionzi ya jua limekuwa jambo la kawaida. Mionzi hii sio tu huifikia ngozi zetu lakini pia huweza kusababisha mabadiliko fulani katika ngozi kupelekea zionekane zimefifia au nyeusi zaidi. Mfano mzuri mtu akitembea juani kwa muda mrefu utaona rangi ya paji la uso liko tofauti na sehemu nyingine za uso au kwa wale wenzetu wanaovaa nguo zinazoacha wazi maeneo ya kifua au mgongo utagundua rangi za maeneo hayo iko tofauti na sehemu zingine za mwili. Hali hii inajulikana kama suntanning. Hutokea pale ngozi inapozalisha zaidi chembe hai zinazofanya kuwa na rangi nyeusi (melanin), ikijaribu kujilinda dhidi ya uharibifu unaoweza kusababishwa na mionzi ya jua. Leo nimekuandalia njia za asili na rahisi ambazo unaweza kuzitumia ili kusaidia kuondoa utofauti wa rangi ya ngozi unaoletwa na mionzi ya jua.
1. Nyanya na Asali.

Mahitaji:- nyanya kubwa 1 na asali (kijiko kikubwa)
Namma ya kufanya:-kuna njia mbili unazoweza kutumia kuandaa remedy hii. (i) chukua nyanya, ikate katikati na uchovye asali upande huo ulioukata kisha anza kupaka sehemu husika.
Au (ii) Chukua nyanya uisage na kisha changanya asali na uanze kupaka. Subiri kwa dakika 15 hadi 20 baada ya hapo nawa maji halafu jikaushe kwa kitambaa safi. Fanya hivi kila siku kupata matokeo yanayo ridhisha.
2. Tango na Asali.

Mahitaji :-
- Tango 1,
- Asali (kijiko 1 cha chai).
Namna ya kufanya:- Saga tango kisha changanya na asali. Paka mchanganyiko huu sehemu iliyoathiriwa, subiri kwa dakika 10 hadi 15 kisha nawa maji. Tumia njia hii mara moja au mbili kila siku.
3. Limao na sukari.

Mahitaji:-
- Limao
- sukari (kijiko kikubwa 1)
Namna ya kufanya:- Kamua limao kupata maji yake kiwango cha kijiko 1 na uchangaje sukari kwenye maji ya limao. Tumia mchanganyiko huu kama scrub katika sehemu iliyoathiriwa kwa ku massage taratibu kwa dakika 2 hadi 3 kisha nawa na maji. Fanya hivi mara kwa mara kupata matokea mazuri zaidi.
4. Apple cider vinega na Baking soda.

- Baking soda (kijiko 1 cha chai)
- vinega (kijiko 1)
Namna ya kufanya:- Changanya baking soda na vinega kupata mchanganyiko ambao sio mzito sana. Paka mchanganyiko huu kama scrub na subiri kwa dakika 5 hadi 10 halafu unawe. Tumia hii mara moja au mbili kwa wiki.
5. Papai

Mahitaji:-
- Papai lililoiva.
Namna ta kufanya:- Chukua papai menya halafu ulisage. Paka mchanginyo huu sehemu husika na usubiri kwa dakika 15 hadi 20 kisha nawa kwa maji ya uvugu uvugu. Paka kila siku au mara kwa mara mpaka utakapopata matokeo yatakayo kuridhisha.
6. Kiazi mviringo.

Mahitaji:-
- Kiazi mviringo 1.
Namna ya kufanya:- kata kiazi katikati, kisha anza kusugua sehemu husika taratibu.
Mbali na njia hizi zilizotajwa, pia inashauriwa kutumia mafuta maalum (sunscreen) ili kuikinga ngozi kutokana na madhara ya mionzi ya jua. Kama una maswali zaidi au maoni kuhusina na mada hii, tunakukaribisha kukomenti hapo chini.
Instagram @gift_reinhard
Related posts
4 Comments
Comments are closed.
HOT TOPICS
Subscribe for newsletter
* You will receive the latest news and updates on your favorite celebrities!
Interviews
Fahamu Zaidi Kuhusu Vazi La Vijiko Kutoka Kwa Harmonize
Mwanamuziki Harmonize ametoa wimbo wake mpya uitwao Attitude, katika music video ya wimbo huu Harmonize ameonekana akiwa amevalia vazi la leather lenye vijiko, uma na visu ( silverware/ cutlery ) Vazi hili limeonekana ku-trend sana wengine wakiwa wanalisifia na wengine kuliponda, tumemtafuta stylist na mbunifu…
Maoni Ya Mbunifu Elisha Red Label Kuhusu Event Ya Miss Tanzania 2020
Tanzania imepata mlimbwende wake mpya ambae ataenda kuliwakilisha Taifa mwakani katika mashindano ya Dunia ya urembo. Tumeona sio mbaya kama tukifanya mahojiano na baadhi ya wabunifu, makeup artist na stylist ambao wametupa maoni yao kuhusu event hii. Hapa tunae mbunifu mkubwa wa mavazi ya kike…
Meet Eddie A Young Male Makeup Artist In A Female Dominated Industry
Anaitwa Eddie ( Makeup By Eddie ) ni mvulana ambae anafanya vizuri katika tasnia ya urembo, Eddie ni makeup artist tofauti na wengine Eddie yeye ni mvulana na kama ambavyo tunajua tasnia hii imetawaliwa sana na wanawake katika bara letu la Africa. Tumepata kujua mawili…
Husiyo Yajua Kuhusu Vaazi
Weekend hii tuliweza shuhudia maonyesho ya mavazi katika Tanzania Summer Festival iliyofanyika pale Double Tree Hotel. Tulivutiwa sana na kazi ya mbunifu chipukizi [pia stylist Vaazi na hivyo kuongea naye mwawili matatu juu ya kazi zake. AFRO: Umetambulika kama stylist anayechipukia na kufanya vizuri, waweza…
… [Trackback]
[…] Info to that Topic: afroswagga.com/urembo/njia-asili-za-kuondoa-utofauti-wa-rangi-ya-ngozi-unaosababishwa-na-mionzi-ya-jua/ […]
… [Trackback]
[…] Read More to that Topic: afroswagga.com/urembo/njia-asili-za-kuondoa-utofauti-wa-rangi-ya-ngozi-unaosababishwa-na-mionzi-ya-jua/ […]
… [Trackback]
[…] Information on that Topic: afroswagga.com/urembo/njia-asili-za-kuondoa-utofauti-wa-rangi-ya-ngozi-unaosababishwa-na-mionzi-ya-jua/ […]
… [Trackback]
[…] Read More here on that Topic: afroswagga.com/urembo/njia-asili-za-kuondoa-utofauti-wa-rangi-ya-ngozi-unaosababishwa-na-mionzi-ya-jua/ […]