Kuwa na rangi tofauti shingoni na mwilini huwa inakera unaonekana mchafu, hata kama una rangi au ngozi nzuri sehemu nyingine lakini ukiwa na shingo nyeusi huwa inaleta picha mbaya. Shingo nyeusi hutokana na kuisahau, unaweza kukuta tunafanya kila nyia kuwa na ngozi nyororo usoni na sehemu nyingine za mwili lakini tunasahau kabisa shingo. Kuna wengine hata mafuta hawapaki shingoni.
Leo tunakuletea njia chache ambazo unaweza kutumia katika kuondoa weusi huu.
- Apple Cider Vinegar
Apple Cider Vinegar husaidia kuzawazisha kiwango cha pH cha ngozi, husaidia kukupa mng’ao wa asili lakini pia huondoa seli za ngozi zilizokufa. Uwepo wa asidi ya malic katika ACV hufanya iwe exfoliator nzuri.

Unachohitaji kufanya ni kuchukua vijiko 2 vya siki ya apple cider na vijiko 4 vya maji na uchanganye vizuri. Paka mchanganyiko huu katika shingo yako na kaa nao kwa dakika 10 kisha unaweza kuosha kwa maji au ukaenda kuoga. Fanya hivi mara kwa mara ili kupata matokeo ya haraka
Note: Hakikisha una moisturizer ngozi yako mara tu ukimaliza kuosha ngozi yako ya ngozi kwa sababu ACV husababisha ngozi kuwa kavu.
- Baking Soda
Baking Soda inasaidia pia katika kuondoa seli za ngozi zilizokufa, kuleta mg’ao lakini pia husadia katika ku-promote circulation

Chukua vijiko 2/3 vya baking soda na maji ya kutosha au limao kutengeneza smooth paste. Paka mchanganyiko wako katika shingo na uache ukauke, ukisha kauka ondoa/bandua mchanganyiko huu kwa kutumia vidole vyako (viloweshe ili usipate maumivu wakati wa kuondoa). Kisha unaweza kuosha kwa maji na kupaka mafuta yako, fanya hivi kila siku ili kupata matokeo kwa haraka.
- Juice Ya Viazi
Kiazi kinasemekana kuwa na bleaching proprieties mbayo inaweza kurahisisha ngozi kwa kiwango kikubwa. Pia husaidia kuondoa weusi katika ngozi yako na kukufanya uwe na rangi moja katika ngozi.

Chukua viazi na upondeponde ukishapata uji wa viazi kamua na chuja ili kupata juice nyepesi, paka kwenye shingo yako na uache ikauke, ikishakauka unaweza kuosha kwa maji ya uvuguvugu. Fanya hivi mara mbili kwa siku kupata matokeo kwa haraka.
- Mtindi
Mtindi una nzymes asili ambayo husadiana na asidi ambayoipo katika limao kutoa matokeo yanayohitajika. Inang’alisha zaidi ngozi na kuifanya iwe laini.

Chukua vijiko 2 vya mtindi na kijiko cha maji ya limao. Changanya viungo hivi viwili na utumie /paka mchanganyiko huu kwenye shingo. Acha kwa muda wa dakika 20 kabla ya kuosha na maji
Related posts
5 Comments
Comments are closed.
HOT TOPICS
Subscribe for newsletter
* You will receive the latest news and updates on your favorite celebrities!
Interviews
Fahamu Zaidi Kuhusu Vazi La Vijiko Kutoka Kwa Harmonize
Mwanamuziki Harmonize ametoa wimbo wake mpya uitwao Attitude, katika music video ya wimbo huu Harmonize ameonekana akiwa amevalia vazi la leather lenye vijiko, uma na visu ( silverware/ cutlery ) Vazi hili limeonekana ku-trend sana wengine wakiwa wanalisifia na wengine kuliponda, tumemtafuta stylist na mbunifu…
Maoni Ya Mbunifu Elisha Red Label Kuhusu Event Ya Miss Tanzania 2020
Tanzania imepata mlimbwende wake mpya ambae ataenda kuliwakilisha Taifa mwakani katika mashindano ya Dunia ya urembo. Tumeona sio mbaya kama tukifanya mahojiano na baadhi ya wabunifu, makeup artist na stylist ambao wametupa maoni yao kuhusu event hii. Hapa tunae mbunifu mkubwa wa mavazi ya kike…
Meet Eddie A Young Male Makeup Artist In A Female Dominated Industry
Anaitwa Eddie ( Makeup By Eddie ) ni mvulana ambae anafanya vizuri katika tasnia ya urembo, Eddie ni makeup artist tofauti na wengine Eddie yeye ni mvulana na kama ambavyo tunajua tasnia hii imetawaliwa sana na wanawake katika bara letu la Africa. Tumepata kujua mawili…
Husiyo Yajua Kuhusu Vaazi
Weekend hii tuliweza shuhudia maonyesho ya mavazi katika Tanzania Summer Festival iliyofanyika pale Double Tree Hotel. Tulivutiwa sana na kazi ya mbunifu chipukizi [pia stylist Vaazi na hivyo kuongea naye mwawili matatu juu ya kazi zake. AFRO: Umetambulika kama stylist anayechipukia na kufanya vizuri, waweza…
… [Trackback]
[…] Read More on that Topic: afroswagga.com/urembo/njia-za-kuondoa-weusi-shingoni/ […]
… [Trackback]
[…] Find More on on that Topic: afroswagga.com/urembo/njia-za-kuondoa-weusi-shingoni/ […]
… [Trackback]
[…] Find More Information here to that Topic: afroswagga.com/urembo/njia-za-kuondoa-weusi-shingoni/ […]
… [Trackback]
[…] Info on that Topic: afroswagga.com/urembo/njia-za-kuondoa-weusi-shingoni/ […]
… [Trackback]
[…] Here you can find 42944 additional Info on that Topic: afroswagga.com/urembo/njia-za-kuondoa-weusi-shingoni/ […]