Hakuna anayefurahia chunusi, na hakuna anayependeza akiwa na chunusi, Chunusi zimekuwa zikiwapata sana watu wenye ngozi za mafuta. Juhudi za kuteketeza mafuta yanayozidi kwenye ngozi zinahitajika kwani ndio chanzo kikuu cha chunusi.
Leo na waletea Apple cider vinegar (siki ya apple) kama kipodozi asilia cha kuzuia na kutibu chunusi.

Apple cider vinegar ina sifa ya kuua bakteria kwa haraka sana, pia ina sifa ya kukausha mafuta kwenye ngozi kwa haraka sana.Ila inashauriwa usitumie mara kwa mara maana kadri unavyokausha mafuta na apple cider vinegar ndivyo tezi za mafuta zinaongeza kasi ya kuzalisha mafuta yaliyokaushwa.
MAHITAJI
- Siki ya apple (apple cider vinegar)
- Maji safi
- Pamba
MATUMIZI
- Osha uso na maji safi,hakikisha uchafu wote umetoa.
- Changanya kifuniko kimoja cha siki kwa vifuniko vitatu vya maji.
- Chovya pamba kwenye mchanganyiko na upake maeneo yenye tatizo,kaa nayo kwa dakika 10 kisha osha.
- Fanya hivyo mara nyingi uwezavyo kwa siku.
- Pia unaweza kupaka na ukalala nayo usiku kucha.
- Hakikisha unapaka moisturiser baada ya kutumia.
Related posts
3 Comments
Comments are closed.
HOT TOPICS
Subscribe for newsletter
* You will receive the latest news and updates on your favorite celebrities!
Interviews
Fahamu Zaidi Kuhusu Vazi La Vijiko Kutoka Kwa Harmonize
Mwanamuziki Harmonize ametoa wimbo wake mpya uitwao Attitude, katika music video ya wimbo huu Harmonize ameonekana akiwa amevalia vazi la leather lenye vijiko, uma na visu ( silverware/ cutlery ) Vazi hili limeonekana ku-trend sana wengine wakiwa wanalisifia na wengine kuliponda, tumemtafuta stylist na mbunifu…
Maoni Ya Mbunifu Elisha Red Label Kuhusu Event Ya Miss Tanzania 2020
Tanzania imepata mlimbwende wake mpya ambae ataenda kuliwakilisha Taifa mwakani katika mashindano ya Dunia ya urembo. Tumeona sio mbaya kama tukifanya mahojiano na baadhi ya wabunifu, makeup artist na stylist ambao wametupa maoni yao kuhusu event hii. Hapa tunae mbunifu mkubwa wa mavazi ya kike…
Meet Eddie A Young Male Makeup Artist In A Female Dominated Industry
Anaitwa Eddie ( Makeup By Eddie ) ni mvulana ambae anafanya vizuri katika tasnia ya urembo, Eddie ni makeup artist tofauti na wengine Eddie yeye ni mvulana na kama ambavyo tunajua tasnia hii imetawaliwa sana na wanawake katika bara letu la Africa. Tumepata kujua mawili…
Husiyo Yajua Kuhusu Vaazi
Weekend hii tuliweza shuhudia maonyesho ya mavazi katika Tanzania Summer Festival iliyofanyika pale Double Tree Hotel. Tulivutiwa sana na kazi ya mbunifu chipukizi [pia stylist Vaazi na hivyo kuongea naye mwawili matatu juu ya kazi zake. AFRO: Umetambulika kama stylist anayechipukia na kufanya vizuri, waweza…
… [Trackback]
[…] Read More on that Topic: afroswagga.com/urembo/ondoa-chunusi-kwa-kutumia-apple-cider-vinegar/ […]
… [Trackback]
[…] Read More on that Topic: afroswagga.com/urembo/ondoa-chunusi-kwa-kutumia-apple-cider-vinegar/ […]
… [Trackback]
[…] Read More Info here on that Topic: afroswagga.com/urembo/ondoa-chunusi-kwa-kutumia-apple-cider-vinegar/ […]