MGONGO ni moja ya kiungo cha mwili ambacho kinahitaji uangalizi mzuri.Bila hivyo huleta tabu hasa pale mgongo unapokuwa hauko katika muonekano mzuri. Uchafu unaoganda kwenye mgongo hupelekea muwasho wa mara kwa mara na mgongo kuwa na mabaka mabaka.
Ukweli ni kuwa jaribu kuangalia mgongo wako na kuona kama unastahili kuwa hivyo na kama haustahili basi chukua hatua kwa kuhakikisha mgongo unakuwa safi na kutafuta tiba ya chunusi au mabakamabaka yaliyo mgongoni mwako.
Unapoufanyia tiba mgongo kwa kutumia sabuni za dawa au lotion utaufanya uwe na muonekano mzuri na hata kuwa huru kuvaa nguo yoyote. Wengi wanashindwa kuvaa nguo za wazi kutokana na muonekano wa ngozi zao za mgongoni kuwa mbaya zenye vipele, chunusi na kupauka.
Madoa kwenye mgongo yamekuwa yakikosesha wengi raha kutokana na suala la utunzaji mgongo halitiliwi maanani kama ilivyo kwenye utunzaji wa uso au miguu.
Tumia brashi laini lenye sababu ya kutosha katika kusugua mgongo wako. Kisha paka mafuta.
Kama huwezi kufikia vizuri mgongo kwa kutumia brashi basi unaweza kuomba msaada ili mradi mgongo utakate na kuwa katika sura ya kupendeza. Wengi wanashindwa kuvaa nguo za wazi kutokana na migongo yao kuwa na sura isiyopendeza.
Ni muhimu ukazingatia usafi wa mgongo ili uwe huru kuvaa nguo za wazi bila kuwa na mashaka kuwa kuna watu wanautazama vibaya mgongo wako na wengine wameanza kucheka.
Aina za Chunusi za mgongoni hazitofautiani sana na zile za usoni kabisaa.
Vifuatavyo ni vile ambavyo unaweza kuandaa nyumbani kwako kutoa chunusi za mgongoni.
1. Scrub ya sukari.
Mahitaji Nusu kikombe cha sukari Nusu kikombe cha Mafuta ya lozi au zaituni ama Mafuta ya Nazi.
Chukua sukari yako nusu changanya na Mafuta vizuri.
Tumia mchanganyiko huu Kama scrub yako kutoa uchafu na taka taka zote kwenye mgongo wako ukiwa unaoga.
Baada ya kuoga, kausha kwa nguo kavu Kisha paka mafuta ya Nazi kidogo Kama kilainishi!
Ufanye Mara ngapi? Ufanye kwa wiki mara mbili.
Kwa nini hii inafanya kazi. Sukari inaweza kukupa mgongo mzuri usio na Chunusi kabisa.
Kufanya scrub kutakusaidia kuondoa ngozi yote iliyokufa ambayo inasababisha hizo Chunusi mgongoni.
Jee unasafishaje mgongo wako?
Imeandikwa na @binturembo
Related posts
1 Comment
Comments are closed.
HOT TOPICS
Subscribe for newsletter
* You will receive the latest news and updates on your favorite celebrities!
Interviews
Fahamu Zaidi Kuhusu Vazi La Vijiko Kutoka Kwa Harmonize
Mwanamuziki Harmonize ametoa wimbo wake mpya uitwao Attitude, katika music video ya wimbo huu Harmonize ameonekana akiwa amevalia vazi la leather lenye vijiko, uma na visu ( silverware/ cutlery ) Vazi hili limeonekana ku-trend sana wengine wakiwa wanalisifia na wengine kuliponda, tumemtafuta stylist na mbunifu…
Maoni Ya Mbunifu Elisha Red Label Kuhusu Event Ya Miss Tanzania 2020
Tanzania imepata mlimbwende wake mpya ambae ataenda kuliwakilisha Taifa mwakani katika mashindano ya Dunia ya urembo. Tumeona sio mbaya kama tukifanya mahojiano na baadhi ya wabunifu, makeup artist na stylist ambao wametupa maoni yao kuhusu event hii. Hapa tunae mbunifu mkubwa wa mavazi ya kike…
Meet Eddie A Young Male Makeup Artist In A Female Dominated Industry
Anaitwa Eddie ( Makeup By Eddie ) ni mvulana ambae anafanya vizuri katika tasnia ya urembo, Eddie ni makeup artist tofauti na wengine Eddie yeye ni mvulana na kama ambavyo tunajua tasnia hii imetawaliwa sana na wanawake katika bara letu la Africa. Tumepata kujua mawili…
Husiyo Yajua Kuhusu Vaazi
Weekend hii tuliweza shuhudia maonyesho ya mavazi katika Tanzania Summer Festival iliyofanyika pale Double Tree Hotel. Tulivutiwa sana na kazi ya mbunifu chipukizi [pia stylist Vaazi na hivyo kuongea naye mwawili matatu juu ya kazi zake. AFRO: Umetambulika kama stylist anayechipukia na kufanya vizuri, waweza…
… [Trackback]
[…] Info to that Topic: afroswagga.com/urembo/ondoa-chunusi-za-mgongo-kwa-kutumia-sukari-na-mafuta-ya-nazi/ […]