Kama tutatakiwa kutaja makeup artist bora Tanzania basi Nuru nae atakuepo kwenye list yetu, ukiachana na kazi yake nzuri lakini pia she is so humble na ana customer care nzuri, tumemjua Nuru kupitia Instagram ambapo anajiita Queennuru_makeup akiwa bado hajafikisha 55k followers ambao anao sasa. Nuru ni professional makeup artist ambae amesomea maswala ya makeup kutokana na kazi yake nzuri amesha fanya kazi na baadhi ya watu maarufu kama Nandy, Zari, Hamisa, Ruby na wengine wengi na haya ni mawili matatu tuliyo yatoa kutoka kwake.
Afroswagga – Ulianza Vipi Mpaka Kufikia Hapa?
Nuru – Baada ya kumaliza masomo yangu ya sekondari,sikuendelea na elimu ya juu,hivyo nikaajiriwa katika kampuni ya SHEARILLUSION hapo ndipo safari yangu ilipoaanza.
Afroswagga – Nini Kiliku Inspire Kufanya Makeup?
Nuru – Nilifanya kazi kwa muda wa miaka 3 na wakati niko katika kampuni hiyo nilichaguliwa kushiriki katika program iitwayo MANJANO DREAMMAKERS ambayo ilinipa elimu ya upambaji(makeup artistry),hivyo safari yangu ya kuanza kupamba ilianza mwaka 2015 mpaka kufikia sasa.
kilichonifanya nifanye kazi hii nni kwasababu nilipenda sana kuona watu wanapendeza kupitia mikono yangu na pia bosi wangu aliona kipaji changu ndio mana alinichagua kushiriki katika kupata elimu ya upambaji.
Celeb Wako wa Kwanza Kufanya Nae Kazi Alikua Ni Nani Na Ilikuaje?
Afroswagga – Celebrity wa kwanza kufanya nae makeup alikuwa Rose Ndauka..,na yeye alipata habari kutoka kwa marafiki zake ambao tayari niliwahi kuwapamba kwahiyo akanipigia simu kuwa nahitaji kufanyiwa makeup ndipo tulipokutana na nikampamba.
Afroswagga – Je Unatumia Local Brands Za Tanzania? Kama Manjano, Eye Lashes Za Watanzania Na Lipsticks? Ubora Wake Upoje
Nuru – Natumia local brands za makeup kama vile LUVTOUCH MANJANO, pia natumia lashes za Lavie na lipstick za Luvtouch pia,na ubora wake ni mzuri sana na hata wateja wangu wanafurahia sana.
Afroswagga – Tofauti ya makeup ya Celeb akiwa anaenda jukwaani na kwenye events kubwa ni IPI?
Nuru – Makeup ya celeb akiwa anaenda kwenye event huwa ni ya kawaida tu yanI simple evening makeup kwa kuwa haiitaji awe na vitu vingi usoni ila akiwa anapanda jukwaani au kwenye show inakuwa kidogo creative kwakuwa atapigwa picha na details za makeup zinapaswa kuonekana vizuri zaidi kwahiyo huwa tunamfanyia contour na pia hata rangi za eyeshadow zinabidi ziwe kidogo zinaonekana.
Afroswagga – umesha wahi kunfanyia MTU makeup na ukakosolewa mitandaoni? Kama yes ulipokeaje ?
Nuru – Nimewahi kufanya makeup na kwenye mitandao nikakosolewa mfano nilipomfanyia simple makeup ZARI ila nilipokea kama changamoto kwenye kazi ambayo imenisaidia kuwa makini zaidi na kufanya kazi nzuri zaidi japo unapopokea kasoro lazima woga uwepo kwa hali ya kibinadamu.
Afroswagga – Umeshawahi Kufanya Makeup Za Fashion Show?
Nuru – Nimewahi kufanya makeup kwa ajili ya fashion show mwaka 2015
Afroswagga – Ni kweli huwa mnawapa watu was kawaida wanafunzi wawahudumie huku nyie mkichagua tu celebs?
Nuru – Si kweli kuwa tunawapa wanafunzi wapambe watu ambao si maarufu kwetu mteja yoyote ni mwenye thamani sana na kwenye saloon yetu wote ambao wanapamba si wanafunzi kwakuwa
kwakuwa tayari wamepitia mafunzo ya upambaji na tunamshukuru Mungu hatujawahi kupata malalamiko kwakuwa wote wanafurahia makeup wanapotoka ila ile tu hulka ya watu kutaka kupambwa na mtu waliyemzoea ipo ila tukiwaelewesha huwa wanakubali kupambwa na mtu yeyote ambaye ni mpambaji saloon kwetu.

Afroswagga – nani unependa kufanya nae kazi mbeleni?
Nuru – Ningependa kufanya kazi hii ya upambaji na celeb kama hawa hapo baadae mfano Wema Sepetu na Elizabeth Michael hawa ni celeb ambao natamani kuwapamba siku moja Mwenyezi Mungu akijaalia
Afroswagga – waambie wa Tanzania kwanini wamchague nuru na sio makeup artist wengine
Nuru – Nawaomba watanzania wanichague mimi kuwafanyia makeup kwasababu;
1.Ninao ujuzi wa kufanya makeup na mpaka sasa nina uzoefu wa miaka 3
2.watakapofanyiwa makaeup watafurahia na hawatajutia kwakuwa kila mtu atabaki na rangi yake kwakuwa mimi ninachofanya si kubadili rangi ya mtu kutoka uhalisia wake ila ni kumpend
kumpendezesha na kumwongezea thamani katika urembo wake
3.Bei zangu ni nafuu kabisa ambazo mtu yoyote anaweza kulipia
Nuru anapatikana sinza africasana ana fanya makeup za aina mbalimbali kamaSend off,Harusi,Kitchen party,Video Shooting,graduation unaweza kumpata hapa pia ☎ 0656442475)
Related posts
5 Comments
Leave a Reply Cancel reply
You must be logged in to post a comment.
HOT TOPICS
Subscribe for newsletter
* You will receive the latest news and updates on your favorite celebrities!
Interviews
Fahamu Zaidi Kuhusu Vazi La Vijiko Kutoka Kwa Harmonize
Mwanamuziki Harmonize ametoa wimbo wake mpya uitwao Attitude, katika music video ya wimbo huu Harmonize ameonekana akiwa amevalia vazi la leather lenye vijiko, uma na visu ( silverware/ cutlery ) Vazi hili limeonekana ku-trend sana wengine wakiwa wanalisifia na wengine kuliponda, tumemtafuta stylist na mbunifu…
Maoni Ya Mbunifu Elisha Red Label Kuhusu Event Ya Miss Tanzania 2020
Tanzania imepata mlimbwende wake mpya ambae ataenda kuliwakilisha Taifa mwakani katika mashindano ya Dunia ya urembo. Tumeona sio mbaya kama tukifanya mahojiano na baadhi ya wabunifu, makeup artist na stylist ambao wametupa maoni yao kuhusu event hii. Hapa tunae mbunifu mkubwa wa mavazi ya kike…
Meet Eddie A Young Male Makeup Artist In A Female Dominated Industry
Anaitwa Eddie ( Makeup By Eddie ) ni mvulana ambae anafanya vizuri katika tasnia ya urembo, Eddie ni makeup artist tofauti na wengine Eddie yeye ni mvulana na kama ambavyo tunajua tasnia hii imetawaliwa sana na wanawake katika bara letu la Africa. Tumepata kujua mawili…
Husiyo Yajua Kuhusu Vaazi
Weekend hii tuliweza shuhudia maonyesho ya mavazi katika Tanzania Summer Festival iliyofanyika pale Double Tree Hotel. Tulivutiwa sana na kazi ya mbunifu chipukizi [pia stylist Vaazi na hivyo kuongea naye mwawili matatu juu ya kazi zake. AFRO: Umetambulika kama stylist anayechipukia na kufanya vizuri, waweza…
… [Trackback]
[…] There you can find 16779 more Information to that Topic: afroswagga.com/urembo/one-on-one-with-makeup-artist-queen-nuru/ […]
… [Trackback]
[…] Read More to that Topic: afroswagga.com/urembo/one-on-one-with-makeup-artist-queen-nuru/ […]
… [Trackback]
[…] Read More here on that Topic: afroswagga.com/urembo/one-on-one-with-makeup-artist-queen-nuru/ […]
… [Trackback]
[…] Here you can find 63012 additional Info to that Topic: afroswagga.com/urembo/one-on-one-with-makeup-artist-queen-nuru/ […]
… [Trackback]
[…] Find More on that Topic: afroswagga.com/urembo/one-on-one-with-makeup-artist-queen-nuru/ […]