Hii style imekuwa maarufu sana, ni style rahisi kuibana lakini pia ni style ambayo unaweza kwenda nayo popote iwe kazini, kwenye mitoko ya kawaida na sehemu nyingine mbalimbali. Kutokana na urahisi wake wa kubana na kuwa useful wengi wetu tunapenda kuitumia mara kwa mara, lakini tuna sahau kwamba style hii inaweza kuharibu nywele zetu.

Namna Ambavyo Style Ya Kidoti Inaharibu Nywele
- Kukata Nywele
Kubana nywele zako kidoti kila siku au mara kwa mara kunaweza kusababisha kukatika kwa nywele, hii hutokana na kuzivuta nywele juu kila siku. Zinaweza kukatika chini pembeni lakini pia hata juu pale unapofungia nywele hasa kama unatumia vibanio vya mpira.
Namna Ambavyo Unaweza Kuondokana Na Kukatika Kwa Nywele Unapobana Kidoti
- Usibane Nywele Zikiwa Nyevu ( Zimeloa)
Nywele zetu huwa dhaifu pale zinapokuwa zimeloa, ukizivuta na kuzibana zinaweza kukatika kwa urahisi, subiri mpaka zikikauka vyema ndipo uzibane.
- Paka mafuta kabla hujazibana
Hii huzifanya nywele kuwa laini na kuteleza pale ambapo zinavutwa, badala ya kukatika zinaweza kuteleza hasa kwa zile ambazo ni laini zaidi au fupi.
- Badilisha style ya nywele zako mara kwa mara
Style zipo nyingi mno kama ni mpenzi wa kubana basi hakikisha unabadilisha sehemu za kubana, unaweza kubana up and low do wakati mwingine jaribu loose styles.
- Tumia Vibanio vya nguo
Achana na vibanio vya mpira tumia vibanio ambavyo vimetengenezwa kutumia nguo na vizuri ni vile ambavyo vimetengenezwa kwa kutumia fabric ya satin.
Related posts
4 Comments
Comments are closed.
HOT TOPICS
Subscribe for newsletter
* You will receive the latest news and updates on your favorite celebrities!
Interviews
Fahamu Zaidi Kuhusu Vazi La Vijiko Kutoka Kwa Harmonize
Mwanamuziki Harmonize ametoa wimbo wake mpya uitwao Attitude, katika music video ya wimbo huu Harmonize ameonekana akiwa amevalia vazi la leather lenye vijiko, uma na visu ( silverware/ cutlery ) Vazi hili limeonekana ku-trend sana wengine wakiwa wanalisifia na wengine kuliponda, tumemtafuta stylist na mbunifu…
Maoni Ya Mbunifu Elisha Red Label Kuhusu Event Ya Miss Tanzania 2020
Tanzania imepata mlimbwende wake mpya ambae ataenda kuliwakilisha Taifa mwakani katika mashindano ya Dunia ya urembo. Tumeona sio mbaya kama tukifanya mahojiano na baadhi ya wabunifu, makeup artist na stylist ambao wametupa maoni yao kuhusu event hii. Hapa tunae mbunifu mkubwa wa mavazi ya kike…
Meet Eddie A Young Male Makeup Artist In A Female Dominated Industry
Anaitwa Eddie ( Makeup By Eddie ) ni mvulana ambae anafanya vizuri katika tasnia ya urembo, Eddie ni makeup artist tofauti na wengine Eddie yeye ni mvulana na kama ambavyo tunajua tasnia hii imetawaliwa sana na wanawake katika bara letu la Africa. Tumepata kujua mawili…
Husiyo Yajua Kuhusu Vaazi
Weekend hii tuliweza shuhudia maonyesho ya mavazi katika Tanzania Summer Festival iliyofanyika pale Double Tree Hotel. Tulivutiwa sana na kazi ya mbunifu chipukizi [pia stylist Vaazi na hivyo kuongea naye mwawili matatu juu ya kazi zake. AFRO: Umetambulika kama stylist anayechipukia na kufanya vizuri, waweza…
… [Trackback]
[…] Find More on to that Topic: afroswagga.com/urembo/style-ya-nywele-ya-kidoti-inavyo-haribu-nywele-zako/ […]
… [Trackback]
[…] Information on that Topic: afroswagga.com/urembo/style-ya-nywele-ya-kidoti-inavyo-haribu-nywele-zako/ […]
… [Trackback]
[…] Find More Info here to that Topic: afroswagga.com/urembo/style-ya-nywele-ya-kidoti-inavyo-haribu-nywele-zako/ […]
… [Trackback]
[…] Info on that Topic: afroswagga.com/urembo/style-ya-nywele-ya-kidoti-inavyo-haribu-nywele-zako/ […]