Inawezekana umenunua unyunyu wako bei ghali kabisa na unaupenda sana lakini kadri siku zinavyozidi kwenda ndivyo ubora wa unyunyu wako unapungua na kukufanya ujiulize kwanini inatokea hivi? Inawezekana ukabadilika harufu sio yote lakini isiwe kama mwanzo au kutokukaa muda mrefu katika mwili kama zamani.
Utajiuliza kwanini hali hii imetokea? utaanza kuwaza labda umeuziwa perfume fake lakini kumbe inawezekana ni sehemu unayo hifadhi perfume yako ndio inasababisha yote haya, Je ni sehemu gani usihifadhi unyunyu wako na kwanini?
- Weka Chupa za Perfume Mbali na Jua
Chupa za manukato nyingi hutengenezwa kwa glasi hivyo ukiweka manukato yako ambapo jua linapiga moja kwa moja (dirishani, dressing table iliyotazamana na mlango au dirisha) inaweza kuharibu haraka manukano, jua linaweza kusababisha joto ndani ya chupa ikapata mvuke na maji maji na quality ya manukato ikapungua. Hakikisha una hifadhi manukano yako sehemu yenye giza.

- Weka Manukato Yako Mbali Na Joto
Basi kukwambia uweke manukato yako gizani sio ndio uweke kwenye kabati ufungie na milango kabisa, hapana. Joto jingi linaweza kuharibu kemikali zilizopo katika perfume na kupunguza ubora wake, hakikisha sehemu unayoweka ina hali nzuri sio joto kali kama ni kabatini au dressing table iwe sehemu ambayo haifikiwi na jua na pia ina ubaridi.
- Weka Perfume Mbali na Unyevu
Wengi wetu huwa tunahifadhi manukato bafuni, ambapo hutumiwa mara nyingi. Kwa bahati mbaya, unyevu kupita kiasi unaweza kuharibu manukato, na wakati umwagaji au kuoga kwa kutumia maji ya moto katika bafu ni mbaya kwa manukato. Kwa kweli, hata vipodozi vilivyohifadhiwa katika bafuni yenye unyevu pia huvunjika kwa haraka zaidi. Hifadhi kipodozi bafuni endapo tu ni bafu lenye uwezo wa kutoa mvuke nje kwa haraka.
Related posts
HOT TOPICS
Subscribe for newsletter
* You will receive the latest news and updates on your favorite celebrities!
Interviews
Fahamu Zaidi Kuhusu Vazi La Vijiko Kutoka Kwa Harmonize
Mwanamuziki Harmonize ametoa wimbo wake mpya uitwao Attitude, katika music video ya wimbo huu Harmonize ameonekana akiwa amevalia vazi la leather lenye vijiko, uma na visu ( silverware/ cutlery ) Vazi hili limeonekana ku-trend sana wengine wakiwa wanalisifia na wengine kuliponda, tumemtafuta stylist na mbunifu…
Maoni Ya Mbunifu Elisha Red Label Kuhusu Event Ya Miss Tanzania 2020
Tanzania imepata mlimbwende wake mpya ambae ataenda kuliwakilisha Taifa mwakani katika mashindano ya Dunia ya urembo. Tumeona sio mbaya kama tukifanya mahojiano na baadhi ya wabunifu, makeup artist na stylist ambao wametupa maoni yao kuhusu event hii. Hapa tunae mbunifu mkubwa wa mavazi ya kike…
Meet Eddie A Young Male Makeup Artist In A Female Dominated Industry
Anaitwa Eddie ( Makeup By Eddie ) ni mvulana ambae anafanya vizuri katika tasnia ya urembo, Eddie ni makeup artist tofauti na wengine Eddie yeye ni mvulana na kama ambavyo tunajua tasnia hii imetawaliwa sana na wanawake katika bara letu la Africa. Tumepata kujua mawili…
Husiyo Yajua Kuhusu Vaazi
Weekend hii tuliweza shuhudia maonyesho ya mavazi katika Tanzania Summer Festival iliyofanyika pale Double Tree Hotel. Tulivutiwa sana na kazi ya mbunifu chipukizi [pia stylist Vaazi na hivyo kuongea naye mwawili matatu juu ya kazi zake. AFRO: Umetambulika kama stylist anayechipukia na kufanya vizuri, waweza…