Wengi wetu tunatumia vipodozi mbalimbali katika ngozi zetu, iwe kwa kuondoa kitu fulani au kukifanya kiwe bora zaidi. Imezoeleka kuwatunanunua vipodozi hivi kwa mazoea iwe kwa kuambiwa au kushauriwa na dakitari.
Mara nyingi huwa tunasahau kusoma lebo na kuona hakuna umuhimu kwa sababu tu kipodozi hiko kimemsaidia fulani au umeshauriwa na mtaalam basi hakina madhara, ni muhimu kusoma lebo ili kujua mambo yafuatayo:
- Kujua Viungo / Ingredients zilizopo katika kipodozi hiko
Ni muhimu kujua kipodozi unachokipaka kina viungo gani na kama ni salama kwa ngozi yako, kwenye vipodozi huwa wanaweka kemikali mbalimbali na nyingine ni kali zinaweza kukusababishia madhara mbeleni. Oh yes inawezekana tusiwe wazuri sana kwenye haya mambo ya kusoma kuhusu kemikali kuna google jaribu ku-google na uone maelezo ya ingredient husika.
Fahamu Vipodozi Vitakavyo Haribu Mwili Wako
- Expiry Date
Ni muhimu kujua kipodozi chako kinaisha muda wake wa kutumika lini, baada ya muda wa kipodozi kuisha inawezekana kisilete matokeo mazuri au pia kukuletea madhara katika ngozi yako.
Mambo Manne (4) Kuhusu Urembo Unapaswa Kujua
- Namna ya kukihifadhi kipodozi chako
Kwenye label huwa kunamaelezo ya namna kipodozi chako kinafaa kuhifadhiwa, unaweza kuambiwa kisikae juani, kiwekwe sehemu ambapo joto lake ni kiasi fulani, ni muhimu kujua haya yote ili kupata matokeo mazuri ya kipodozi katika ngozi yako.

- Namna ya kukitumia
Kwenye lebo kuna maelezo kama unaweza kukuta kimeandikwa kitumiwe mara mbili kwa siku asubuhi na wakati wa kulala, vingine havitakiwi kulala navyo, lakini pia kuna ambavyo unaambiwa utumie direct kwenye tatizo kama upake kwenye chunusi au doa tu bila kupaka kwingine ambapo hakuna madhara. Ni muhimu kujua haya yote.
- Msimu wa kupaka kipodozi chako
Kuna vipodozi huwa vinapakwa kwa msimu labda wakati wa baridi au joto, inabidi ujue kipodozi unacho kitumia kinafaa kutumika katika msimu au hali gani ya hewa, japo si product nyingi ambazo huandikwa lakini unaweza kujua kwa kusoma ingredients zilizopo na zinafaa kutumiwa katika hali ipi.
Related posts
2 Comments
Comments are closed.
HOT TOPICS
Subscribe for newsletter
* You will receive the latest news and updates on your favorite celebrities!
Interviews
Fahamu Zaidi Kuhusu Vazi La Vijiko Kutoka Kwa Harmonize
Mwanamuziki Harmonize ametoa wimbo wake mpya uitwao Attitude, katika music video ya wimbo huu Harmonize ameonekana akiwa amevalia vazi la leather lenye vijiko, uma na visu ( silverware/ cutlery ) Vazi hili limeonekana ku-trend sana wengine wakiwa wanalisifia na wengine kuliponda, tumemtafuta stylist na mbunifu…
Maoni Ya Mbunifu Elisha Red Label Kuhusu Event Ya Miss Tanzania 2020
Tanzania imepata mlimbwende wake mpya ambae ataenda kuliwakilisha Taifa mwakani katika mashindano ya Dunia ya urembo. Tumeona sio mbaya kama tukifanya mahojiano na baadhi ya wabunifu, makeup artist na stylist ambao wametupa maoni yao kuhusu event hii. Hapa tunae mbunifu mkubwa wa mavazi ya kike…
Meet Eddie A Young Male Makeup Artist In A Female Dominated Industry
Anaitwa Eddie ( Makeup By Eddie ) ni mvulana ambae anafanya vizuri katika tasnia ya urembo, Eddie ni makeup artist tofauti na wengine Eddie yeye ni mvulana na kama ambavyo tunajua tasnia hii imetawaliwa sana na wanawake katika bara letu la Africa. Tumepata kujua mawili…
Husiyo Yajua Kuhusu Vaazi
Weekend hii tuliweza shuhudia maonyesho ya mavazi katika Tanzania Summer Festival iliyofanyika pale Double Tree Hotel. Tulivutiwa sana na kazi ya mbunifu chipukizi [pia stylist Vaazi na hivyo kuongea naye mwawili matatu juu ya kazi zake. AFRO: Umetambulika kama stylist anayechipukia na kufanya vizuri, waweza…
… [Trackback]
[…] Read More to that Topic: afroswagga.com/urembo/umuhimu-wa-kusoma-lebo-katika-vipodozi/ […]
… [Trackback]
[…] Here you will find 7768 additional Info on that Topic: afroswagga.com/urembo/umuhimu-wa-kusoma-lebo-katika-vipodozi/ […]