Usafi haubagui, iwe mkaka au mdada lazima uwe nadhifu haijalishi upo nyumbani, kazini, ama barabarani, Moja ya jambo ambalo wakaka wengi tumeona hushindwa kufanikisha ni usafi wakucha za mikononi na miguuni. Waweza kuonana na mkaka mtanashati kapendeza lakini ukatazama kucha ukaishia kushangazwa na uchafu uuonao.
Ili kutekeleza usafi wa kucha kwa wakaka, haihitaji vitu vingi. Vipo vya msingi ambavyo waweza kuwa navyo nakujitengeneza kila weekend nyumbani, navyo ni:
NAIL CUTTER
Wanaume wengi hufanya kazi za suluba hivyo uchafu huingia kuchani. Hakikisha hukosi nail cutter nyumbani au hata utembeapo katika mkoba wako. Kucha chafu huleta madhara makubwa ikiwemo magonjwa ya tumbo. Pia haifai mguuni kutoboa socks kisa makucha marefu, shughulika mwana wane.
NAIL FILE
Ni kifaa ambacho hutumika kusawazishia kucha. Kwa baadhi ya nail cutters huwa nazo ila yafaa ukiwa nacho pia ili kuziweka kucha zako zikiwa na muonekano unaofaa.
CUTICLE SCISSORS
Katika kucha huwa twaona ngozi zikiota pembezoni mwa kucha na wengi huzing’ata lakini kiutaalamu. Kifaa hiki kitakusaidia kuondoa ngozi hizo na kucha kubaki zinapendeza.
Pia yafaa kuosha mikono na miguu kila siku pale ushikapo uchafu wa aina yoyote ile. Waweza jisafisha vizuri pindi uogapo ili kuonda maradhi na uchafu uufanyao kucha kudumaa na kutovutia.
Na yashauriwa kunywa maji mengi maana husaidia katika kucha. Tumeona wakaka wengi wakibanduka ngozi za chini ya kucha. Suluhisho la hili si kuzibandua ngozi hizo hadi utokwe damu abli kunywa maji mengi tu kila sku nautajionea mabadiliko
Imeandikwa na @willibard_jr
Related posts
HOT TOPICS
Happiness Magese Akionyesha Wanawake Warefu Namna Ya Kuwa Stylish: Kwa wanawake warefu huwa… https://t.co/VZ1jH2zJUg
FollowHappiness Magese Akionyesha Wanawake Warefu Namna Ya Kuwa Stylish: Kwa wanawake warefu huwa… https://t.co/689j7Yjcn0
FollowSubscribe for newsletter
* You will receive the latest news and updates on your favorite celebrities!
Interviews
Maoni Ya Mbunifu Elisha Red Label Kuhusu Event Ya Miss Tanzania 2020
Tanzania imepata mlimbwende wake mpya ambae ataenda kuliwakilisha Taifa mwakani katika mashindano ya Dunia ya urembo. Tumeona sio mbaya kama tukifanya mahojiano na baadhi ya wabunifu, makeup artist na stylist ambao wametupa maoni yao kuhusu event hii. Hapa tunae mbunifu mkubwa wa mavazi ya kike…
Meet Eddie A Young Male Makeup Artist In A Female Dominated Industry
Anaitwa Eddie ( Makeup By Eddie ) ni mvulana ambae anafanya vizuri katika tasnia ya urembo, Eddie ni makeup artist tofauti na wengine Eddie yeye ni mvulana na kama ambavyo tunajua tasnia hii imetawaliwa sana na wanawake katika bara letu la Africa. Tumepata kujua mawili…
Husiyo Yajua Kuhusu Vaazi
Weekend hii tuliweza shuhudia maonyesho ya mavazi katika Tanzania Summer Festival iliyofanyika pale Double Tree Hotel. Tulivutiwa sana na kazi ya mbunifu chipukizi [pia stylist Vaazi na hivyo kuongea naye mwawili matatu juu ya kazi zake. AFRO: Umetambulika kama stylist anayechipukia na kufanya vizuri, waweza…
Feza Kessy Atuelezea Kuhusu Fashion & Style Zake
Feza Tadei Kessy ni Muimbaji, Muigizaji lakini pia ni mtunzi wa nyimbo lakini pia Fezza ni former beauty queen ambapo mwaka 2005 alikuwa Miss Dar City Centre, Miss Ilala & Miss Tanzania Runner up. Lakini pia alishawahi kuwepo katika Reality Tv Show – Big Brother Africa. Kwa…