Umeshawahi kuwa na ngozi nzuri week nzima kisha unaanza jumatatu yako na ngozi ambayo huelewi? unaanza kujiuliza hizi rashes nimetoa wapi au mbona ngozi yangu imeharibika ghafla? Hii hutokana na mambo kadhaa ambayo tunayafanya weekend na yanaweza kuwa chanzo cha skin breakout
- Kuto Kulala Kwa Masaa 8-9
Tunajua kutokupata usingizi wa kutosha kunaweza kuzidisha kuonekana kwa aging signs na kupunguza skin elastic ambayo itapelekea kuzidi kuonekana kwa makunyanzi ya ngozi pamoja na uneven skin pigmentation. So jaribu kupata usingizi wa kutosha na usiangalie Tamthilia au kukesha weekend nzima
- Kula Junk Food
Weekend tunatoka tunaenda ku-enjoy maisha unaweza kujikuta siku nzima umekula un-healthy food zenye mafuta au sukari nyingi, hii inaweza kupelekea kusababisha chunusi usoni, hakikisha una kula vyakula vya aina hii kwa kiasi usizidishe.
- Kulala Na Makeup
Inawezekana umetoka na marafiki ukapaka makeup yako umerudi umechoka unaamua kulala nazo hivyohivyo, hii pia inaweza kupelekea upate skin breakout, hakikisha ukirudi unaondoa makeup yako kisha ulale.
- Kuacha Nywele Zikagusa Uso Wako
Weekend tunajiachia unaenda kutengeneza nywele unaziachi, umepakwa mafuta ya nywele zinagusa uso wako zile kemikali zilizopo kwenye vipodozi vya vywele vinaingia kwenye ngozi yako na kuleta madhara, hakikisha style ya nywele unayoiweka hata kama ni ya kuziachia sio kubana basi nywele hazigusi uso.
- Kuto Kupaka Sunscreen
Inawezekana unatoka au hutoki unahisi hauna haja ya kupaka sun screen, hakikisha ukitoka au usipotoka hata kama upo ndani unapaka suncreen yako ili kukuepusha na breakouts.
Tuwatakie weekend njema na jitahidi kulinda ngozi yako
Related posts
HOT TOPICS
Subscribe for newsletter
* You will receive the latest news and updates on your favorite celebrities!
Interviews
Fahamu Zaidi Kuhusu Vazi La Vijiko Kutoka Kwa Harmonize
Mwanamuziki Harmonize ametoa wimbo wake mpya uitwao Attitude, katika music video ya wimbo huu Harmonize ameonekana akiwa amevalia vazi la leather lenye vijiko, uma na visu ( silverware/ cutlery ) Vazi hili limeonekana ku-trend sana wengine wakiwa wanalisifia na wengine kuliponda, tumemtafuta stylist na mbunifu…
Maoni Ya Mbunifu Elisha Red Label Kuhusu Event Ya Miss Tanzania 2020
Tanzania imepata mlimbwende wake mpya ambae ataenda kuliwakilisha Taifa mwakani katika mashindano ya Dunia ya urembo. Tumeona sio mbaya kama tukifanya mahojiano na baadhi ya wabunifu, makeup artist na stylist ambao wametupa maoni yao kuhusu event hii. Hapa tunae mbunifu mkubwa wa mavazi ya kike…
Meet Eddie A Young Male Makeup Artist In A Female Dominated Industry
Anaitwa Eddie ( Makeup By Eddie ) ni mvulana ambae anafanya vizuri katika tasnia ya urembo, Eddie ni makeup artist tofauti na wengine Eddie yeye ni mvulana na kama ambavyo tunajua tasnia hii imetawaliwa sana na wanawake katika bara letu la Africa. Tumepata kujua mawili…
Husiyo Yajua Kuhusu Vaazi
Weekend hii tuliweza shuhudia maonyesho ya mavazi katika Tanzania Summer Festival iliyofanyika pale Double Tree Hotel. Tulivutiwa sana na kazi ya mbunifu chipukizi [pia stylist Vaazi na hivyo kuongea naye mwawili matatu juu ya kazi zake. AFRO: Umetambulika kama stylist anayechipukia na kufanya vizuri, waweza…