Kuna msemo unaosema “you are what you eat”, yes huu msemo hauja kosea kama ambavyo inajulikana ukila vyakula vya ajabu ajabu vina haribu mwili wako basi ni sawasawa na ngozi hasa ngozi ya mafuta, sio tu vinazidi kufanya ngozi yako kuwa na mafuta lakini pia zinaweza kusababisha matatizo ya ngozi kama chunusi,white heads na black heads etc. Lakini habari nzuri ni kwamba unaweza kuepuka haya yote kama utaondoa baadhi ya vyakula katika diet yako, well waswahili husema “mtaka cha uvunguni shurti uiname” kama unahitaji kitu inatakiwa ukubali ku strive for it.
leo tunawaletea baadhi ya vyakula ambavyo unatakiwa kukaa mbali navyo kama ngozi yako ni ya mafuta
Vyakula Venye/ Vilivyo Tengenezwa Na Maziwa Mengi
Vinaweza vikawa ni vyakula vyako pendwa au vinaulazima kutumika katika maandalizi ya chakula lakini tuamini hivi vyakula vina matokeo makubwa ambayo yanaongeza mafuta katika ngozi yako, unaweza kupunguza au kuacha kabisa kutumia vyakula kama Ice cream, butter,butter milk etc.
Kahawa Au Chai
Kahawa na chai vina dyhdrate mwili wako hii inaweza kupelekea uzalishaji wa mafuta na kusababisha chunusi na vipele vidogo vidogo, unaweza kupunguza kunywa chai na kahawa na kunywa maji mengi na handmade juice.
Pombe
Pombe ni kama kahawa ina dydrate mwili wako ambapo inaweza kupelekea uzalishaji wa mafuta mwilini na kusababisha ngozi kuendelea kuwa na mafuta lakini pia kupata skin issue kama chunusi.
Sukari
Kutumia sukari husababisha spike katika blood sugar levels. Hii inaongoza kwa uzalishaji wa insulini zaidi, ambayo, kwa upande wake, husababisha tezi za kuzalisha mafuta zaidi. Hii inapelekea kuwa na ngozi yenye mafuta ambayo matokeo yake huleta chunusi . Epuka kula mikate, jamu, vyakula vya unga, na pipi. Tumia sukari za asili, zilizopo katika matunda na mboga, kwa kiasi.
chumvi
Chumvi ya ziada inaweza kusababisha uhifadhi wa maji na kuvimba. Inaweza pia kusababisha ongezeko la oil levels katika ngozi, pale ambapo mwili unapo jaribu kupambana na maji machafu yanayosababishwa kutokana na matumizi makubwa ya chumvi. Epuka kula chumvi ya ziada au vyakula vyenye chumvi nyingi.
Related posts
3 Comments
Comments are closed.
HOT TOPICS
Subscribe for newsletter
* You will receive the latest news and updates on your favorite celebrities!
Interviews
Fahamu Zaidi Kuhusu Vazi La Vijiko Kutoka Kwa Harmonize
Mwanamuziki Harmonize ametoa wimbo wake mpya uitwao Attitude, katika music video ya wimbo huu Harmonize ameonekana akiwa amevalia vazi la leather lenye vijiko, uma na visu ( silverware/ cutlery ) Vazi hili limeonekana ku-trend sana wengine wakiwa wanalisifia na wengine kuliponda, tumemtafuta stylist na mbunifu…
Maoni Ya Mbunifu Elisha Red Label Kuhusu Event Ya Miss Tanzania 2020
Tanzania imepata mlimbwende wake mpya ambae ataenda kuliwakilisha Taifa mwakani katika mashindano ya Dunia ya urembo. Tumeona sio mbaya kama tukifanya mahojiano na baadhi ya wabunifu, makeup artist na stylist ambao wametupa maoni yao kuhusu event hii. Hapa tunae mbunifu mkubwa wa mavazi ya kike…
Meet Eddie A Young Male Makeup Artist In A Female Dominated Industry
Anaitwa Eddie ( Makeup By Eddie ) ni mvulana ambae anafanya vizuri katika tasnia ya urembo, Eddie ni makeup artist tofauti na wengine Eddie yeye ni mvulana na kama ambavyo tunajua tasnia hii imetawaliwa sana na wanawake katika bara letu la Africa. Tumepata kujua mawili…
Husiyo Yajua Kuhusu Vaazi
Weekend hii tuliweza shuhudia maonyesho ya mavazi katika Tanzania Summer Festival iliyofanyika pale Double Tree Hotel. Tulivutiwa sana na kazi ya mbunifu chipukizi [pia stylist Vaazi na hivyo kuongea naye mwawili matatu juu ya kazi zake. AFRO: Umetambulika kama stylist anayechipukia na kufanya vizuri, waweza…
… [Trackback]
[…] Info on that Topic: afroswagga.com/urembo/vyakula-vya-kuepuka-kama-una-ngozi-ya-mafuta/ […]
… [Trackback]
[…] Information to that Topic: afroswagga.com/urembo/vyakula-vya-kuepuka-kama-una-ngozi-ya-mafuta/ […]
… [Trackback]
[…] Find More Info here on that Topic: afroswagga.com/urembo/vyakula-vya-kuepuka-kama-una-ngozi-ya-mafuta/ […]