VIJANA wanapofikia umri wa kubalehe, moja kati ya dalili wanazokumbana nazo ni kuota nywele sehemu za siri ikiwamo kwapani. Wengi wao wamekuwa wakishindwa kujiweka katika hali ya usafi hivyo kujikuta wakitoa harufu kali ya jasho. Jambo hilo huwakwaza watu wengi na hivyo kujikuta wakijitenga /wakitengwa bila kujua sababu.
Kunuka kikwapa ni tatizo kubwa katika mwili wa binadamu. Tatizo hili husababishwa na bakteria wanaovutiwa na jasho au unyevunyevu chini ya kwapa. Sasa basi, kuna njia nyingi ambazo watu wengi huzitumia ili kwapa liwe na harufu nzuri, kavu na safi. Zifuatazo ni mbinu 9 za kuondoa / kuzuia kikwapa
1.Wengine hutumia njia za kisasa ambazo ni pamoja na kupaka deodoranti au pafyumu zinazosaidia kuondoa harufu mbaya mwilini.
2. Lakini kama hiyo haitoshi, kuna njia za asili Kabisa zinazoweza kuzuia harufu ya kwapa ambazo ni pamoja na kupaka kipande cha limao kwenye kwapa na kuacha lipate hewa safi ili kuua vijidudu na kutoa tezi za jasho kuondoa harufu mbaya.
3.Kuvaa nguo safi zenye nyuzinyuzi za asili kama pamba, hariri na sufi zitasaidia kufyonza unyevu na kuliacha kwapa lako kuwa kavu, safi na bila harufu mbaya.
4. Kuoga kila siku na kusafisha nguo kwa maji safi kunasaidia kuua bakteria na ambao husababisha harufu mbaya.
5. Pia kunywa maji mengi kila siku kunakusaidia kutoa sumu mwilini na hivyo kupunguza harufu mbaya ya kwapa.
6. Njia nyingine inayoshauriwa ni kuhakikisha kuwa unaosha kwapa mara kwa mara kwa kutumia sabuni zenye dawa (medicated soaps).
7. Aidha, kupunguza kula chakula chenye viungo vingi hasa vitunguu. Inasemekana kuwa kula vitunguu vingi kunachangia mwili kutoa harufu kali.
Licha ya pafyumu na spray kusaidia kuondoa harufu mbaya mwilini, hii si dawa endelevu kwani baada ya muda harufu inaweza kurudi palepale hivyo ni vema kutumia njia za asili kukabiliana na hali hiyo. Pafyumu haiwezi kutibu tatizo moja kwa moja.
8.Pia inashauriwa kuwa baada ya kuoga jifute kwa taulo au kitambaa safi na usiache unyevu unyevu ambao huwavutia bakteria kukua katika maeneo yaliyojificha (yenye mikunjo).
9.Mbinu nyingine ni kujitahidi kunyoa nywele za kwapa mara kwa mara na kuepuka kukaa sehemu zenye joto kupita kiasi kwa muda mrefu.
Jee ni mbinu gani uliyokuwa ukiitumia hapo Kabla? Imeandikwa Na @binturembo
Related posts
1 Comment
Comments are closed.
HOT TOPICS
We need to have some sort of bima ila for enjoyment. Yaani wanakata ka % ka mshahara kako unakua na card ukienda se… https://t.co/W9oDoaN2YY
FollowSubscribe for newsletter
* You will receive the latest news and updates on your favorite celebrities!
Interviews
Fahamu Zaidi Kuhusu Vazi La Vijiko Kutoka Kwa Harmonize
Mwanamuziki Harmonize ametoa wimbo wake mpya uitwao Attitude, katika music video ya wimbo huu Harmonize ameonekana akiwa amevalia vazi la leather lenye vijiko, uma na visu ( silverware/ cutlery ) Vazi hili limeonekana ku-trend sana wengine wakiwa wanalisifia na wengine kuliponda, tumemtafuta stylist na mbunifu…
Maoni Ya Mbunifu Elisha Red Label Kuhusu Event Ya Miss Tanzania 2020
Tanzania imepata mlimbwende wake mpya ambae ataenda kuliwakilisha Taifa mwakani katika mashindano ya Dunia ya urembo. Tumeona sio mbaya kama tukifanya mahojiano na baadhi ya wabunifu, makeup artist na stylist ambao wametupa maoni yao kuhusu event hii. Hapa tunae mbunifu mkubwa wa mavazi ya kike…
Meet Eddie A Young Male Makeup Artist In A Female Dominated Industry
Anaitwa Eddie ( Makeup By Eddie ) ni mvulana ambae anafanya vizuri katika tasnia ya urembo, Eddie ni makeup artist tofauti na wengine Eddie yeye ni mvulana na kama ambavyo tunajua tasnia hii imetawaliwa sana na wanawake katika bara letu la Africa. Tumepata kujua mawili…
Husiyo Yajua Kuhusu Vaazi
Weekend hii tuliweza shuhudia maonyesho ya mavazi katika Tanzania Summer Festival iliyofanyika pale Double Tree Hotel. Tulivutiwa sana na kazi ya mbunifu chipukizi [pia stylist Vaazi na hivyo kuongea naye mwawili matatu juu ya kazi zake. AFRO: Umetambulika kama stylist anayechipukia na kufanya vizuri, waweza…
… [Trackback]
[…] Find More on on that Topic: afroswagga.com/urembo/zijue-mbinu-9-za-kuondoa-harufu-ya-kikwapa/ […]